BONGOCLAN Tanzania

Website yetu ipo katikamatengenezo

Copyright © BongoClan Tanzania™ | Published By Gooyaabi Templates | Powered By Blogger
Design by WebSuccessAgency | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com

HABARI ZILIZOSOMWA SANA WIKI HII

Wema ni kweli anavuta Bangi???

Staa wa Bongo Movie, Komediani kipenzi cha wengi Bongo, Majuto Athuman ‘Mzee Majuto’, anadaiwa kuzama kwa mara nyingine kwenye penzi la msichana mbichi anayekadiriwa kuwa na umri sawa na mjuu wake.

Akizungumza na gazeti la Ijumaa Wikienda, wikiendi iliyopita, mke wa Mzee Majuto aitwaye Aisha Yusuf alikiri kuwa mumewe amenasa kwa ‘kibinti’ chenye umri wa miaka 18.
Aisha alidai kwamba, Mzee Majuto anaishi na binti huyo kama mke na mume, jambo ambalo watu wamekuwa wakimshangaa na kuhoji kwa nini anatoka na mtoto mdogo kiasi hicho wakati ana watoto wakubwa wenye uwezo wa kuzaa msichana kama huyo na akawa mjukuu wake.
“Kinachonichosha mimi kwa nini anafanya hivyo wakati yeye ni kioo cha jamii?
“Watu wengi wanatakiwa kujifunza mengi kupitia kwake, maana tangu aoe hata sisi hatujafurahishwa na jambo hilo ingawa kweli ni uamuzi wake.
“Kingine amekuwa hakai tena hapa nyumbani (Tanga) na kuna kipindi unapita hata mwezi tunawasilia kwenye simu tu labda mtoto aumwe ndiyo atapita tu na siyo kukaa.
“Sijui mzee wangu anafanya hivyo kwa nini maana sasa ana zaidi ya miaka 60 na kama mtoto mimi sasa hivi nina umri wa miaka 35 kwake bado mimi mdogo sana na nina umri wa watoto wake wa kuzaa sasa huyo aliyemuoa si ni mjukuu wake kabisa?
“Mimi naona aibu tu kama familia ingawa dini kweli inaruhusu lakini si kwa mtoto kama yule,” alisema Aisha kwa uchungu.
Baada ya kumsikia mkewe, gazeti hilo lilimtafuta Mzee Majuto ili azungumzie ishu hiyo ambapo simu yake ilipokelewa na msichana mwenye sauti nyororo huku akidai kwamba mzee Majuto amelala apigiwe baadaye.
“Mimi ni mke wake mdogo, Mzee Majuto amelala, nafikiri jaribu kupiga baadaye anaweza kuwa ameamka na utaweza kuzungumza naye vizuri,” alisema.
Mzee Majuto alipotafutwa baadaye, simu yake iliita bila kupokelewa.
Baadhi ya wasanii waliozungumza na gazeti hili kwa sharti la kutotajwa majina yao walilaani kitendo cha Mzee Majuto kuwa na binti huyo kwani umri wake umeenda.