Katika harakati za kulinyakua Jimbo la Mikumi wilayani Kilosa, Mkoa wa Morogoro kwa tiketi ya chama chake cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), mwanamuziki mkongwe wa muziki wa Kizazi Kipya, Joseph Haule almaarufu Profesa Jay (pichani) ameendelea kupasua anga kwenye jimbo hilo akifungua matawi mapya na kuhamasisha watu kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura.