Msanii wa filamu na vichekesho, Musa Kitale jioni ya leo akizungumza
kwenye studio za Magic FM,kipindi cha Afrika Kabisa kwenye kipengele
cha African Movies, alisema wazi kuwa hawakubali kabisa bongo movies
kwani wanapenda kurudia rudia na kukopi filamu za nje na kusisitiza
hata akiziangalia filamu zao huwa haoni jipya na hazina ubunifu.
Akaendelea kufafanua kuwa yeye sio mwana Bongo Movies na wala hayupo
karibu nao kwani anaogopa kuwaambukizwa ‘kaugonjwa’ kakukopi kopi kitu
mbacho aliwahi kumutahadharisha hata alikuwa lafiki yake wa karibu
marehemu Sharo Milionea asiwe karibu nao.
Kitale alikuwa pamoja na Stan Bakora wakielezea ujio wa filamu ya
SAFARA HASARA ambayo ndio ya mwisho ya Kitale na Sharo Milionea
kurekodi pamoja.
Akielezea filamu hiyo Kitale amesema japo kuwa filamu hiyo wamerekodi
mwaka 2012 lakini hadi sasa hakuna hata filamu moja ya kibongo ambayo
ina ubunifu kuifunika filamu.
Filamu ya SAFARA HARASA itaingia sokoni mwezi huu tarehe 20 mwaka huu.