BONGOCLAN Tanzania

Website yetu ipo katikamatengenezo

Copyright © BongoClan Tanzania™ | Published By Gooyaabi Templates | Powered By Blogger
Design by WebSuccessAgency | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com

HABARI ZILIZOSOMWA SANA WIKI HII

Wema ni kweli anavuta Bangi???

Meneja wa Bia chapa Serengeti Primium Lager,  Rugambo Rodney, (kulia) akiongea kwa njia ya simu na mshindi wa sita wa Limo Bajaji, Ramadhani Abubakar, katika shindano la Tutoke na Serengeti lililofanyika katika makao makuu ya kampuni hiyo jijini Dar es Salaam. Kulia ni msimamizi toka bodi ya michezo ya kubahatisha, Baraka Majid.

Meneja wa Bia chapa Serengeti Primium Lager, Rugambo Rodney, (katikati) akiongea kwa njia ya simu na mshindi wa sita wa Limo Bajaji, Ramadhani Abubakar, katika shindano la “Tutoke na Serengeti” lililofanyika jana makao makuu ya kampuni hiyo jijini Dar es Salaam. Kulia ni msimamizi toka bodi ya michezo ya kubahatisha, Bw. Baraka Majid na kushoto ni msimamizi toka PriceWater Cooper, Golder Kamuzora
Meneja wa Bia chapa Serengeti Premium Lager, Rugambo Rodney, (katikati) akibonyeza kitufe wakati wa kutafuta mshindi wa sita wa Limo Bajaji, katika shindano la “Tutoke na Serengeti” lililofanyika makao makuu ya kampuni hiyo Chang'ombe jijini Dar es Salaam. Kulia ni msimamizi toka bodi ya michezo ya kubahatisha, Baraka Majid na kushto ni msimamizi toka PriceWater Cooper, Golder Kamuzora. 

SERENGETI BREWERIES LTD
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
MKAZI WA MWANZA ASHINDA BAJAJI YA SITA YA PROMOSHENI YA TUTOKE NA SERENGETI
Bajaji ya sita ya kampeni ya Tutoke na Serengeti, safari hii itaelekea mkoani Mwanza baada ya bwana. Ramadhan Abubakar kutangazwa kuwa mshindi wa Limo Bajaj, kufuatia ushiriki wake yakinifu tangu kuanza kwa kampeni hii.
Akiongea kwa njia ya simu, Abubakar (28) ambaye ni fundi umeme na mkazi wa Nyamagana, Mwanza alielezea furaha yake baada ya kuelezwa na SBL kwamba ameshinda Limo Bajaj mpya katika kampeni ya Tutoke na Serengeti…. “Aisee Mungu ni Mwema,…alitahamaki,… asante sana kwa kunipa habari hii njema sikutarajia kushinda kabisa.”
Baada kuulizwa ni kwa namna gani ataitumia bajaji  aliyoshinda katika shughuli zake za kila siku , alisema ataitumia Bajaji hii kwa shughuli za usafirishaji. Mwakazi aliongeza kwamba bajaji hiyo itamsaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza kipato cha familia kwa zaidi ya asilimia 50 huku akiwa na lengo la kujiendeleza kitaaluma kwenye ufundi umeme.
Akiongea na vyombo ya habari leo katika makao makuu ya SBL yaliyoko Chang’ombe Dar es salaam, Meneja chapa wa Serengeti Premium Lager Mr. Rugambo Rodney alisema “ Mshindi wetu wa sita wa Limo Bajaj nae anatoka nje ya Dar es salaam kuashiria kwamba kampeni hii imepokelewa vizuri mikoani  kinyume na ilivyozoeleka na watu wengi kwamba  kampeni za namna hii ni za wakazi wa Dar tu. Rodney aliongeza kuwa kwa sasa imebaki nafasi moja ambayo ni ya Mtoko wa mbugani huku akiwahimiza wateja kutumia mwezi huu wa wapendanao kuwa “Surprise” na kutoa zawadi ya “Mtoko wa mbugani kwa wenza wao ndani ya hifadhi ya taifa ya Serengeti.
Kwa upande mwingine ujumbe kutoka BPESA wataalam wa teknolojia ambao katika promosheni hii wanahusika na usambazaji wa fedha kwa washindi kupitia njia ya simu maeneo mbalimbali hapa nchini, imethibitisha kuwalipa fedha taslim washindi wa kila wiki.
Ili kushiriki katika promosheni hii, mteja anatakiwa awe na umri wa miaka 18, anunue Serengeti Premium Lager na aangalie chini ya kizibo ambapo atakutana na namba maalum anazotakiwa kuzituma kwa njia ya sms kwenda 15317. Kadiri unavyoshiriki mara nyingi ndivyo unavyojiweka katika nafasi ya ushindi.