BONGOCLAN Tanzania

Website yetu ipo katikamatengenezo

Copyright © BongoClan Tanzania™ | Published By Gooyaabi Templates | Powered By Blogger
Design by WebSuccessAgency | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com

HABARI ZILIZOSOMWA SANA WIKI HII

Wema ni kweli anavuta Bangi???

Meneja mipango ya biashara, matukio na uhamasishaji  wote wa kampuni ya Serengeti Breweries Limited Bw. Denis Tairo akizungumza na wateja wa bia ya Serengeti Premium Lager wakati wa uzinduzi kampeni ya tuzo ya dhahabu ya ubora wa thamani ya Monde Selection kwa wakazi wa kanda ya ziwa jijini Mwanza ambapo bia ya Serengeti Premium Lager ya SBL imetuzwa medali tatu za dhahabu kutoka kwenye viwanda vyake vyote vitatu; cha Dar es salaam, Mwanza na Moshi kwa mwaka 2015. Uzinduzi huo ulifanyika katika baa ya “The dreams” iliyopo Kona ya Bwiru jijini Mwanza.

Mdau wa bia ya Serengeti Premium Lager Ben Rockman akijaribu kuitambua bia ya Serengeti Premium Lager ,aliposhiriki kwenye shindano la kumtafuta “Serengeti Masta” wa baa ya “The dreams” ya jijini Mwanza wakati wa kusherekea uzinduzi kampeni ya tuzo ya dhahabu ya ubora wa thamani ya Monde Selection ambapo kwa mwaka huu bia ya Serengeti Premium Lager toka SBL imejinyakulia medali tatu za dhahabu kutokana na ubora wake. Kauli mbiu ya kampeni hii ikiwa ni “SERENGETI PREMIUM LAGER. TUNAIJUA BIA NA HII NDIO YENYEWE”.

Wafanyakazi wa kampuni ya Serengeti Brewieries Limited wakiwa na Mabalozi wa kinywaji hicho wakati wa kutambulisha Tuzo ya Dhahabu ya Monde inayotambulika kimataifa baada ya bia ya Serengeti Premium Lager kukidhi viwango vya juu vya ubora katika hafla iliyofanyika katika Baa ya Oriental ,Majengo mjini Moshi mwishoni mwa wiki.

Mkazi wa Kona ya Bwiru jijini Mwanza Bw. Godfrey Urio akishiriki katika shindano la kumpata “Serengeti Masta” ambapo mpenzi wa kinywaji hicho anatakiwa aitambue bia ya Serengeti Premium lager na kushiriki maswali ili kushinda. Shindano hilo lilifanyika wakati wa kusherekea uzinduzi kampeni ya tuzo ya dhahabu ya ubora wa thamani ya Monde Selection kwa wakazi wa kanda ya ziwa jijini Mwanza ambapo kwa mwaka huu bia ya Serengeti Premium Lager toka SBL imejinyakulia medali tatu za dhahabu kutokana na ubora wake. Shindano hilo litafanyika Tanzania nzima na kuibua Mshindi mmoja kwa kila kanda na mwisho kumuibua wa kitaifa. Kauli mbiu ya kampeni hii ikiwa ni “TUNAIJUA BIA NA SERENGETI PREMIUM LAGER NDIO YENYEWE”.