BONGOCLAN Tanzania

Website yetu ipo katikamatengenezo

Copyright © BongoClan Tanzania™ | Published By Gooyaabi Templates | Powered By Blogger
Design by WebSuccessAgency | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com

HABARI ZILIZOSOMWA SANA WIKI HII

Wema ni kweli anavuta Bangi???

Mbunge wa viti Maalum Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia UVCCM Mkoa wa Kigoma, Zainab Katimba (aliyevaa Gum Boots), akiwaongoza Vijana wenzake katika zoezi la kufanya usafi, ambapo wamefanya usafi katika eneo la Hospitali ya Maweni.

Mbunge wa viti Maalum Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia UVCCM Mkoa wa Kigoma, Zainab Katimba (aliyevaa Gum Boots), akiwaongoza Vijana wenzake katika zoezi la kufanya usafi, ambapo wamefanya usafi katika eneo la Hospitali ya Maweni.


UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) mkoa wa Kigoma wakiongozwa na Mbunge wa Vijana Mh. Zainab Katimba wameunga mkono agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli kwa kufanya usafi  katika hospitali ya Rufaa Mkoa wa Kigoma Maweni.
Usafi huo ambao umeenda sambamba na kugawa zawadi mbali mbali kwa wagonjwa hospitalini hapo, ambazo ni sabuni na vifaa mbali mbali vya usafi juisi na biskuti umelenga kuunga mkono zoezi la kufanya usafi katika siku ya maadhimisho ya siku ya Uhuru.
Akizungumza hospitalini hapo Bi. Katimba alisema kuwa, wao kama vijana wameamua kuwa mfano kwa kuanza kutekeleza agizo hilo kwa kufanya usafi hospitalini hapo, Soko la Mwanga lililopo mjini Kigoma pamoja na kutembelea kituo cha watoto yatima ambapo wamefanya usafi kituoni hapo na kugawa zawadi mbalimbali kwa watoto ikiwemo vyakula.
Alisema lengo la kufanya usafi ni kuhakikisha magonjwa mbali mbali kama kipindupindu yanatokomezwa kwa kuweka maeneo yote kuwa safi. "Leo tumeamua kuanza na hili zoezi rasmi, lakini zoezi hili ni endelevu" Katimba alisema.
Aidha Mhe. Katimba alitoa wito kwa vijana wote tanzania nzima wajikite kuunga mkono jitihada zinazofanywa na serikali ya awamu ya tano katika kuboresha maisha ya watanzania. Mhe. Katimba ametoa agizo kwa vijana wote Tanzania nzima kuwa mstari wa mbele katika kufanya usafi siku ya tarehe 9 Dec 2015.