Mshindi
wa mwisho wa shindano la Serengeti Masta kwa wakazi wa kanda ya ziwa
Said Kanolo, akionyesha pesa zake alizokabidhiwa, kwenye shindano la
mwisho la kumtafuta Serengeti Masta wa mwisho wa kanda hiyo ambalo
lililofanyika katika baa ya Shooters iliyopo barabara ya Airport jijini
Mwanza. Shindano hilo limemalizika rasmi kwa wakazi wa kanda ya ziwa
likiwa limetembelea baa mbalimbali katika kanda hiyo na kuwafikia wateja
wengi zaidi walioweza kuitambua ladha ya bia ya Serengeti Premium Lager
na kutuzwa zawadi mbalimbali pamoja na fedha taslim.
Mshindi
wa jumla wa shindano la Serengeti Masta Said Kanolo (katikati)
akifurahi na wadau wa bia ya Serengeti Premium Lager, wakati wa shindano
la mwisho la Serengeti Masta kwa wateja wa kanda ya ziwa lililofanyika
katika baa ya Shooters iliyopo barabara ya Airport jijini Mwanza.
Kampeni hiyo ya Serengeti Masta imedumu katika kanda hiyo kwa takriban
muda wa miezi (2) sasa ikiwakutanisha wateja na meneja wa bia hiyo
katika kujifunza kwa undani kuhusiana na bia hiyo ambapo zawadi
mbalimabli zilipatikana.
Mshindi
wa jumla washindanola Serengeti Masta kwa wakazi wa kanda ya ziwa Said
Kanolo (kushoto) akipokea fedha taslim Tsh. 100,000/= kutoka kwa Afisa
mauzo wa Kampuni ya bia ya Serengeti Joan Semguruma, (kulia) wakati wa
shindano la mwisho kwa kanda ya ziwa la bia hiyo lililofanyika katika
baa ya Shooters iliyopo Barabara ya Airport jijini Mwanza. Ushindi wa
jumla wa Bw. Kanolo kwa wateja wa kanda ya ziwa umekuja baada ya
kuwashinda wateja wengi walioshiriki katika kutambua ladha halisi ya bia
hiyo na kuielezea kwa undani ambapo mwanzo wa Kampeni alishinda Tsh.
50,000/= pamoja na zawadi nyingine kutoka bia ya Serengeti Premium Lager
katika baa ya Cross parkjijini Mwanza nakufanikiwakutingafainali.
Kampeni hii imezunguka katika baa mbalimbali za kanda ya ziwa
ikiwaburudisha wateja wa bia hiyo na kuwafundisha wahudumu wa baa
mbalimbali juu ya utoaji huduma kwa wateja.
Wadau
wa bia ya Serengeti Premium lager wakigonga cheers, ndani ya baa ya
Shooters iliyopo barabara ya Airport jijini Mwanza wakati wa shindano la
mwisho la kumtafuta Serengeti Masta wa jumla kwa mikoa ya kanda ya ziwa
katika baa hiyo. Kampeni ya “Serengeti Masta” imedumu katika kanda hiyo
kwa takriban miezi miwili na imezunguka baa kwa baa kusaka washindi
mbalimbali wanaotambua ladha halisi ya bia hiyo lakini pia imetoa elimu
kwa wateja wake kuhusiana na chapa hiyo namba moja kutoka SBL.