Mkazi
wa Magomeni jijini Dar es salaam Sam Stima akifurahia zawadi yake ya
fulana kutoka kwa balozi wa bia ya Serengeti Premium Lager Razani
Kapalatu wakati wa promosheni ya Serengeti Masta iliyofanyika katika
baa ya Ulaya Ulaya iliyopo Manzese jijini Dar es salaam. Promosheni
hiyo ya bia ya Serengeti Premium Lager imefanikiwa kuwafikia wateja na
wahudumu wa baa mbalimbali katika kipindi cha miezi miwili ikitoa
zawadi ya fedha taslim na elimu kuhusiana na ubora wa bia yake.
Mshereheshaji
wa shindano la Serengeti Masta Razani Kapalatu( akionyesha kiasi cha
Tsh. 50,000/= alichomkabidhi mshindi wa shindano la Serengeti Masta
ambaye aliitambua ladha halisi ya bia ya Serengeti Premium Lager wakati
wa promosheni hiyo iliyofanyika katika baa ya Ulaya Ulaya iliyopo
Manzese jijini Dar es salaam. (Kushoto) ni mteja aliyeibuka “Serengeti
Masta” wa baa hiyo ambaye alifahamika kwa jina la Doris Frances.
Mshindi
wa shindano la Serengeti Masta Doris Frances (kushoto) kwenye picha ya
pamoja na marafiki zake mara baada ya kuibuka bingwa wa kuitambua
ladha halisi ya bia ya Serengeti na kukabidhiwa zawadi ya Tsh 50,000
wakati wa promosheni hiyo iliyofanyika mwishoni wa wiki katika baa ya
Ulaya Ulaya iliyopo Manzese jijini Dar es Salaam.
Mshereheshaji
wa shindano la Serengeti Premium Lager liliopewa jina la “Serengeti
Masta” Razani Kapalatu akiwa pamoja na mabalozi wa bia ya Serengeti
premium Lager ambao kwa pamoja walitoa maelezo kwa wateja wa bia hiyo
waliofika kushiriki katika shindano la kumtafuta Serengeti Masta ndani
ya baa ya Ulaya Ulaya iliyopo Manzese jijini Dar es salaam mwishoni mwa
wiki. Shindano hilo limedumu jijini Dar na mikoani kwa takriban muda wa
miezi miwili sasa na kuweza kuzifikia baa mbalimbali ambapo zawadi
mbalimbali kama fedha taslim, fulana na bia za bure zimekuwa zikitolewa
katika kuwahamasisha wateja wa bia hiyo kuendelea kuwa pamoja.