BONGOCLAN Tanzania

Website yetu ipo katikamatengenezo

Copyright © BongoClan Tanzania™ | Published By Gooyaabi Templates | Powered By Blogger
Design by WebSuccessAgency | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com

HABARI ZILIZOSOMWA SANA WIKI HII

Wema ni kweli anavuta Bangi???





Mmoja wa wateja wa bia ya Serengeti aliyefahamika kwa jina la Mwasiti Masauni (wa kwanza kulia) akichagua karatasi ya maswali ili kujiwezesha kushinda kiasi cha Tsh. 50,000/= (Elfu Hamsini), wakati wa shindano la kumtafuta Serengeti Masta wa baa ya Meridan iliyopo Kinondoni jijini Dar es Salaam. Shindano hilo ambalo linazunguka baa kwa baa jijini Dar es salaam na mikoani lina lengo la kuwatafuta washindi mbalimbali wanaoweza kuitambua ladha halisi ya bia ya Serengeti na hatimaye kuwazawadia.




Mteja wa bia ya Serengeti Mwasiti Masauni (wa kwanza kulia) akishiriki katika shindano la kutambua ladha ya bia ya Serengeti linalojulikana kama “Serengeti Masta” lililofanyika katika baa ya Meridian iliyopo Kinondoni jijini Dar es salaam. Shindano hilo ambalo linaendelea hivi sasa jijini Dar es salaam na mikoani linalenga kumpata mshindi mmoja kwa kila baa inayotembelewa anayeweza kuitambu ladha halisi ya bia ya Serengeti. (Kushoto) ni mabalozi wa bia ya Serengeti waliosindikiza shindano hilo.




Mshindi wa shindano la Serengeti Masta Bw. Salum Ally (wa kwanza kushoto) akipokea kitita chake cha Tsh. 50,000/= toka kwa balozi wa bia ya Serengeti baada ya kuitambua ladha halisi ya bia ya Serengeti kwenye shindano la kumtafuta Serengeti Masta wa baa ya Meridian iliyopo Kinondoni jijini Dar es salaam. Wakishuhudia zawadi hiyo (wa pili kushoto) ni Meneja wa hoteli ya Meridian Bw. Sem Mkini na mshiriki mwenza wa shindano hilo (wa kwanza kulia) Mwasiti Masauni.