Mshereheshaji
wa shindano la Serengeti Premium Lager liliopewa jina la “Serengeti
Masta” Richard Godwin akitoa maelekezo kwa washiriki wa shindano hilo la
mwisho kwa wilaya ya Ilala lililofanyika mwishoni mwa wiki katika baa
ya Havana Park iliyopo Segerea jijini Dar es salaam. Shindano la
Serengeti Masta limedumu jijini Dar na mikoani kwa takriban muda wa
miezi mitatu sasa na kuweza kuzifikia baa zaidi ya 200 ambapo zawadi
mbalimbali kama fedha taslim, fulana na bia za bure zimekuwa zikitolewa
katika kuwahamasisha wateja wa bia hiyo kuendelea kuwa pamoja.
Mshereheshaji
na mratibu wa mashindano ya kumsaka Serengeti Masta Richard Godwin
akionyesha kiasi cha fedha taslim zilizowaniwa na “Serengeti Masta” wa
wilaya ya Ilala wakati wa mpambano huo uliofanyika mwishoni mwa wiki
katika baa ya Havana iliyopo Segerea jijini Dar es salaam. Kampeni hiyo
imefikia kikomo baada ya kuzunguka katika baa mbalimbali jijini na
mikoani katika kuwasaka washindi waliotambua ladha halisi ya bia ya
Serengeti ambapo pia ilifanikiwa kuwafikia wahudumu zaidi ya mia tano
katika baa tofauti tofauti waliopewa somo la utoaji huduma kwa wateja.
Mmoja
wa washiriki wa shindano la “Serengeti Masta” Godfrey Dickson
akishiriki kuchanganya ladha tofauti za chapa za bia mbalimbali kutoka
Kampuni ya bia ya Serengeti wakati wa shindano la kumtafuta Serengeti
Masta wa wilaya ya Ilala lililofanyika katika baa ya Havana Park iliyopo
Segerea jijini Dar es salaam. Shindano la” Serengeti Masta”
lilianzishwa mahususi kwa ajili ya kurudisha shukrani kwa wateja wa bia
ya Serengeti Premium Lager mara baada ya bia hiyo kushinda
kinyang’anyiro cha bia ya kimataifa yenye viwango bora katika tuzo za
“monde selection” za mwaka huu.
Mkazi
wa Segerea Raymond Sanga akishiriki kuchanganya ladha tofauti za bia
mbalimbali kutoka Kampuni ya bia ya Serengeti wakati wa shindano la
kumtafuta Serengeti Masta wa wilaya ya Ilala lililofanyika mwishoni mwa
wiki katika baa ya Havana Park iliyopo Segerea jijini Dar es salaam.
Pamoja nae ni balozi wa bia hiyo Blessing Zakaria. Shindano la Serengeti
Masta limefikia kikomo jijini Dar es salaam ambapo limefanikiwa
kuwaibua washindi mbalimbali kutoka katika wilaya zake zote tatu.
Mshindi
wa jumla wa shindano la Serengeti Masta kwa wilaya ya Ilala Raymond
Sanga akionyesha fedha taslim Tsh. 100,000/= alizopokea toka kwa
Msimamizi wa mauzo ya Kampuni ya bia ya Serengeti kanda ya Segerea
Nicholaus Charles Mafundo wakati wa shindano la mwisho la kumtafuta
“Serengeti Masta” wa jumla wa wilaya hiyo lililofanyika mwishoni mwa
wiki katika baa ya Havana Park iliyopo Segerea jijini Dar es salaam.
---
Kampeni
ya “Serengeti Masta” iliyokua ikiendeshwa na Kampuni ya bia ya
Serengeti chini ya udhamini wa bia yake namba moja ya Serengeti Premium
Lager, imefikia kilele jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki baada ya
kampeni hiyo kuzunguka kwa muda wa miezi mitatu katika miji ya Arusha,
Mbeya, Mwanza na Morogoro.
Katika
kufunga Kampeni hiyo kwa kishindo, kwa kushirikiana mameneja wa bia ya
Serengeti Premium Lager, walijipanga kuwafikia mashabiki wengi zaidi wa
bia hiyo ambapo iliwalazimu kufanya shindano la “Serengeti Masta”
katika baa tatu zilizopo jijini Dar es salaam kwa siku tofauti.
Sherehe
hizo ambazo zilionekana kuwafurahisha mashabiki wengi wa bia ya
Serengeti Premium Lager, ziliambatana na burudani ya mziki, zawadi za
fedha taslim, fulana na bia za bure.
Baadhi
ya baa za jijini Dar es Salaam, ambazo zilizochaguliwa kuimalizia
promosheni hiyo ni pamoja na Kisuma iliyopo Temeke, Zambezi Ubungo na
Havana Park ya Segerea.
Akiizungumzia
promosheni hiyo mmoja wa wateja maarufu wa bia ya Serengeti Premium
Lager aliyehudhuria shindano la “Serengeti Masta” katika baa ya Kisuma
iliyopo Temeke jijini Dar es Salaam, Bw. Salehe Kitwana, aliipongeza
Kampuni ya bia ya Serengeti na mameneja wa bia hiyo, kwa kuibua kampeni
ambayo imeweza kuwahamasisha wahudumu wa baa mbalimbali jijini Dar es
Salaam na mikoani katika utoaji huduma bora kwa wateja wa bia hiyo,
sambamba na kuwazawadia fedha taslim washiriki mbalimbali walioweza
kuitambua ladha halisi ya bia ya Serengeti baada ya bia hiyo
kushindanishwa na bia nyingine tano zinazotengenezwa na Kampuni ya bia
ya Serengeti (SBL).
“Promosheni
kama hii inawaunganisha mashabiki na kuwafanya waipende bia yao zaidi
na zaidi pia nadhani huu ni mfano wa kuigwa na bia nyingine zinaweza
kujifunza mengi kutokana na promosheni kama hii”.alisema Bw. Salehe
Naye
Meneja Masoko wa bia ya Serengeti Premium Lager Bi. Anitha Msangi
alisema,”Kampeni hii imekuwa ikiendeshwa kwa muda wa miezi mitatu sasa
na kuanza kupamba moto baada ya mashabiki kuipokea kwa mikono miwili na
kuifanya kuwa maarufu.
Alisisitiza
kuwa, shindano la “Serengeti Masta” ni moja kati ya kampeni kubwa
ambazo zimeweza kufanikiwa kiutekelezaji kwa mwaka huu, ikiwa ni moja ya
kazi kubwa zilizofanywa na Kampuni ya bia ya Serengeti.
Bi.
Msangi pia alitumia nafasi hiyo kuwashukuru wateja wote wa bia ya
Serengeti Premium Lager mameneja wa baa mbalimbali walioshiriki kwenye
kampeni hii na wafanyakazi wote wa SBL nchi nzima kwa kuwaunga mkono na
kushiriki kikamilifu katika kufanikisha zoezi zima la kampeni hiyo.
Aliongeza
kuwa pamoja na ushiriki wa wateja kuwa mzuri lakini pia wamefanikiwa
kuongeza mauzo ya bia ya Serengeti kufikia kiwango kikubwa kuliko hapo
awali kwa mwaka huu.
Tafiti
mbalimbali zilizofanywa na SBL katika kipindi cha miezi mitatu ya
kampeni hii imedhihirisha kuwa kampeni hiyo haikufaidisha tu kampuni ya
bia ya Serengeti bali pia baa zaidi ya 4000 zilizotembelewa na shindano
hilo nchi nzima katika kipindi chote cha miezi mitatu.
Vilevile
kampeni hiyo imeibua washindi mbalimbali waliopewa cheo cha Serengeti
Masta ambao walijizolea fedha taslim na bia za bure, fulana na zawadi
mbalimbali.
“Namshukuru
Mungu na sisi pia tumebahatika kuweza kuwa sehemu ya kampeni hii kabla
ya kufikia tamati na ninajiona kama mwenye bahati sana” alisema Meneja
wa baa ya Kisuma Thomas Kimaro ambaye alihojiwa na waandishi wa habari
wakati wa shindano la mwisho la Serengeti Masta lililofanyika kwenye baa
yake.
Kimaro
aliipongeza Kampuni ya bia ya Serengeti kwa kuwa mashuhuri wa kubuni
mambo mapya kila kukicha na kuwasihi kuendelea kuleta promosheni kama
hizi kwa kuwa zinaongeza mauzo ya bia hizo kwenye baa zao.
Kampeni
ya Serengeti Masta ilianzishwa mahususi kwa ajili ya kurudisha shukrani
kwa wateja wa bia ya Serengeti Premium Lager mara baada ya bia hiyo
kushinda kinyang’anyiro cha bia ya kimataifa yenye viwango bora katika
tuzo za “monde selection” za mwaka huu.