BONGOCLAN Tanzania

Website yetu ipo katikamatengenezo

Copyright © BongoClan Tanzania™ | Published By Gooyaabi Templates | Powered By Blogger
Design by WebSuccessAgency | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com

HABARI ZILIZOSOMWA SANA WIKI HII

Wema ni kweli anavuta Bangi???

Mkazi wa Tegeta Kibaoni aliyetambulika kwa jina la Libelius Ochungo (Katikati) akipokea zawadi ya mfuko na fulana toka kwa balozi wa bia ya Tusker Veronica Mbilinyi (Kulia) wakati wa promosheni ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani ambayo ilifanyika katika baa ya Family iliyopo Tegeta jijini Dar es salaam. Baa hiyo ilitangazwa kama mshindi wa wiki wa promosheni hiyo inayoendeshwa na bia ya Tusker toka Kampuni ya bia ya Serengeti. Promosheni hii inaendelea pia katika mikoa ya Arusha, Mbeya, Mwanza, Moshi na Morogoro. (Kushoto) ni Mshereheshaji wa Promosheni hiyo Gadner Habash.
Mkazi wa Tegeta Kibaoni na mpenzi wa bia ya Tusker Bi. Leonarda Shayo akiifurahia zawadi yake ya mfuko na fulana aliyokabidhiwa pale promosheni ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani ilipofunga kambi ndani ya baa ya Family iliyopo Tegeta jijini Dar. Baa hiyo iliibuka mshindi wa wiki wa promosheni hiyo ambayo inadhaminiwa na bia ya Tusker toka Kampuni ya bia ya Serengeti. Akikabidhi zawadi hiyo (Kulia) ni Balozi wa bia ya Tusker Veronica Mbilinyi na (Kushoto) ni mshereheshaji wa promosheni hiyo Gadner Habash.

Mfanyabiashara na Mkazi wa Tegeta, Bw. Tungalaza Andrew akipokea zawadi yake ya fulana toka kwa Meneja Masoko wa bia ya Tusker Nandi Mwiyombella wakati wa promosheni ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani wikiendi ya Ijumaa iliyofanyika katika baa ya Family iliyopo Tegeta jijini Dar es salaam. Baa hiyo iliibuka baa ya wiki kwenye promosheni hiyo inayoendeshwa na bia ya Tusker toka Kampuni ya bia ya Serengeti.
Mkazi wa Tegeta, Uwanja wa Upanga ambaye pia ni Mwalimu wa shule ya Sekondari Max Richard akijiandaa kupokea zawadi ya fulana toka kwa Meneja Masoko wa bia ya Tusker Bi. Nandi Mwiyombella (Kulia) wakati wa promosheni ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani katika kiwanja cha baa ya Family iliyopo Tegeta jijini Dar es salaam. Baa hiyo iliibuka baa ya wiki kwenye promosheni hiyo inayoendeshwa na bia ya Tusker yenye lengo la kuzihamasisha baa mbalimbali za mitaa inayotuzunguka kufanya kweli kwenye utoaji huduma kwa wateja. Promosheni hiyo ya nchi nzima inaendelea pia katika mikoa ya Arusha, Mwanza, Moshi, Morogoro na Mbeya.
Mkazi wa Mtaa wa Yombo-Temeke, Bi. Asha Bakari akipokea zawadi yake ya fulana toka kwa Afisa Masoko anayejifunza kwa vitendo toka Kampuni ya bia ya Serengeti Bw. Josephat Shelukindo katika hafla ya kuipongeza baa ya Kisuma iliyopo Temeke jijini Dar baada ya baa hiyo kuibuka mshindi wa wiki kwenye promosheni ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani Kiwanjani inayodhaminiwa na bia ya Tusker toka Kampuni ya bia ya Serengeti. Promosheni hii ya Tusker imejikita katika kuziunga mkono baa mbalimbali za mitaa inayotuzunguka ili kuhakikisha kuwa zinatambulika kwa wateja wa eneo husika na kufanya kweli kwenye utaoji wa huduma.