Mpenzi
wa kinywaji cha Tusker na mkazi wa Baracuda Tabata Rehema Jumbe
(katikati) akipokea zawadi yake ya Mfuko wenye fulana sambamba na bia za
bure toka kwa Balozi wa kinywaji hicho Veronica Mbilinyi (Kushoto)
katika hafla ya kuipongeza baa ya Baracuda ya Tabata jijini Dar es
salaam mara baada ya baa hiyo kuibuka mshindi wa wiki kwenye kampeni ya
Fanyakweli Kiwanjani inayoendeshwa na bia ya Tusker. Bi. Rehema
aliimwagia sifa bia hiyo kuwa ni laini na haichoshi.
Mkazi wa Tabata Magengeni, Gerald William (36) akipokea zawadi yake ya fulana toka kwa balozi wa bia ya Tusker Veronica Mbilinyi (Kushoto) katika
hafla ya kuipongeza baa ya Baracuda iliyopo Tabata jijini Dar es salaam
ambayo iliibuka mshindi wa wiki kwenye kampeni ya Fanyakweli Kiwanjani
inayoendeshwa na bia ya Tusker. (Kulia) mshereheshaji wa kampeni hiyo Gadner Habash. Kampeni hii inaendelea mikoani pia ambapo itawafikia wakazi wa; - Arusha, Mbeya, Mwanza, Moshi na Morogoro.
Dj
wa redio Efm, anayefahamika kwa jina la Dj Con akifungua burudani ya
muziki ndani ya baa ya Baracuda iliyopo Tabata jijini Dar es salaam
wakati wa hafla ya kuipongeza baa hiyo iliyoibuka mshindi wa wiki kwenye
kampeni inayoendelea ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani. Kampeni hii
inaendelea mikoani pia ambapo itawafikia wakazi wa; - Arusha, Mbeya,
Mwanza, Moshi na Morogoro.
Mpenzi
wa bia ya Tusker Salima Ally akifurahia zawadi yake ya fulana
aliyopokea toka kwa mtangazaji wa redio Efm na mshereheshaji wa kampeni
ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani Gadner Habash wakati kampeni hiyo
ilipofunga kambi katika
baa ya Check point Chanika kuipongeza baa hiyo iliyoibuka mshindi wa
wiki kwenye shindano la Fanyakweli Kiwanjani linaloendeshwa na bia ya
Tusker. Nia ya kampeni hiyo ni kuhamasiha baa mbalimbali za mitaa
inayotuzunguka kufanya kweli wanapotoa huduma kwa wateja wao.