Mkuu
wa kitengo cha Kuhamasisha Masoko kwa wateja toka Kampuni ya bia ya Serengeti
Bw. Alfa Mria akizungumza na wateja wa bia ya Serengeti Premium Lager wakati wa
uzinduzi rasmi wa tuzo ya ubora wa thamani ya Monde Selection ambapo bia ya
Serengeti Premium Lager ya SBL imetuzwa medali ya dhahabu mwaka huu wa 2015.
Sherehe ya kuzindua ushindi huo kwa wateja ilifanyika katika baa yaToroka Uje iliyopo
Kimara jijini Dar es salaam.
Meneja
Masoko wa Kampuni ya bia ya Serengeti Bi. Anitha Msangi (Kushoto) pamoja na Meneja
Mauzo wa kampuni bia ya Serengeti kanda ya Dar es salaam Bw. Godson Tezura wakizindua
rasmi tuzo ya ubora wa thamani ya Monde Selection kwa wateja wa Dar es salaam ambapo
bia ya Serengeti Premium Lager toka SBL imetuzwa medali tatu za dhahabu mwaka huu
kutoka viwanda vyake vyote vitatu; cha Dar es salaam, Mwanza na Moshi kwa mwaka
2015. Sherehe ya kuzindua ushindi huo ilifanyika katika baa ya Toroka Uje iliyopo
Kimara jijini Dar es salaam.
Wafanyakazi
wa Kampuni ya bia ya Serengeti wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa kusherekea
uzinduzi rasmi wa tuzo ya ubora wa thamani ya Monde Selection kwa wateja ambapo
bia ya Serengeti Premium Lager imetuzwa medali tatu za dhahabu kila moja kutoka
katika viwanda vyake mwaka huu wa 2015. Sherehe ya kuzindua ushindi huo kwa wateja
ilifanyika katika baa ya Toroka Uje iliyopo Kimara jijini Dar es salaam.
Meneja
Masoko wa Kampuni ya bia ya Serengeti Bi. Anitha Msangi akifafanua jambo kwa waandishi
wa habari kuhusu uzinduzi wa tuzo ya ubora wa thamani ya Monde Selection ambapo
bia ya Serengeti Premium imetuzwa medali tatu za dhahabu kutoka katika viwanda vyake vyote kwa mwaka
huu wa 2015 pamoja na kufafanua zaidi kuhusu shindano jipya la Serengeti Masta
lilioanza kutimua vumbi katika baa yaTorokaUje iliyopo Kimara jijini Dar.
Meneja
Mauzo wa bia ya Serengeti Premium kanda ya Dar es salaam Bw. Godson Tezura akizungumza
na waandishi wa habari kuhusiana na ubora wa bia hiyo ambao ana amini ndio uliopelekea
ushindi wa tuzo ya kimataifa ya Monde Selection ambapo kwa mwaka huu bia hiyo imetuzwa
medalitatu za dhahabu katika viwanda
vyake vyote vitatu. Bw. Tezura alisisitiza jinsi gani wateja wa wakubwa na
wadogo watafaidika na kampeni hii ya Serengeti Masta.
Msimamizi
wa Mauzo wa Kampuni ya bia ya Serengeti kanda ya Ubungo Bw. Victor Mhindi akikabidhi
zawadi ya polo shirt pamoja na fedha taslim Tsh 50,000/= kwa mkazi wa Kimara mwisho
Bi. Sharifa Shaaban mara baada ya mkazi huyo kuibuka mshindi wa shindano la
“Serengeti Masta wa baa ya Toroka Uje” linaloendeshwa na SBL kupitia kinywaji chake
cha Serengeti Premium Lager wakati wa kusherekea uzinduzi wa tuzo ya ubora wa thamani
ya Monde Selection ambapo bia ya hiyo imetuzwa medali tatu za dhahabu kwa mwaka
huu wa 2015. Sherehe hiyo ilifanyika katika baa ya Toroka Uje iliyopo Kimara jijini
Dar essalaam. Shindano hili litafanyika
Tanzania nzima na kuibua Serengeti Masta wa kanda na mwisho wa taifa. Kauli
mbiu ya kampeni ni TUNAIJUA BIA NA SERENGETI PREMIUM LAGER NDIO YENYEWE