BONGOCLAN Tanzania

Website yetu ipo katikamatengenezo

Copyright © BongoClan Tanzania™ | Published By Gooyaabi Templates | Powered By Blogger
Design by WebSuccessAgency | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com

HABARI ZILIZOSOMWA SANA WIKI HII

Wema ni kweli anavuta Bangi???


Wahudumu wa baa ya MK-Kinondoni wakipozi katika picha wakati wa sherehe za kuipongeza baa hiyo iliyoibuka mshindi wa mwisho wa shindano la Fanyakweli Kiwanjani lilofanyika siku ya jumamosi jijini Dar.

Meneja vipoozeo na mwonekano toka kampuni ya bia ya Serengeti Bw. Baraka Mandara (kulia) akikabidhi zawadi ya mfuko wenye zawadi kwa Bw. Eric Medard ambaye alijumuika na wapenzi wengine wa bia ya Tusker kuipongeza baa ya MK iliyopo Kinondoni iliyoibuka mshindi wa mwisho wa Kampeni ya Fanyakweli Kiwanjani jijini Dar.

Mameneja wa bia ya Tusker toka Serengeti wakipozi katika picha ya pamoja baada ya kujumuika na wapenzi wa bia hiyo katika baa ya MK iliyopo Kinondoni jijini Dar ambayo iliibuka mshindi wa mwisho wa shindano la Fanyakweli Kiwanjani linaloendeshwa chini ya udhamini wa bia ya Tusker. Toka kulia ni Meneja chapa ya Tusker Bi. Sialouise Shayo, na (katikati) ni Meneja masoko wa familia ya Tusker Bi. Anitha Msangi, (kushoto) ni Meneja vipoozeo na mwonekano wa SBL Bw. Baraka Mandara.

Meneja wa chapa ya Tusker toka kampuni ya bia ya Serengeti, Bi. Sialouise Shayo (kulia) akitoa zawadi ya fedha taslim Tsh.100,000/= kwa wahudumu wa baa ya MK iliyopo Kinondoni jijini Dar wakati wa sherehe za kuipongeza baa hiyo ambapo baa hiyo illibuka mshindi wa mwisho wa shindano la Fanyakeli Kiwanjani. Zawadi hiyo ni kwa ajili ya wahudumu wote wa baa hiyo baada ya kufanya kweli kwa kutoa huduma nzuri kwa wateja wa Tusker waliofika kiwanjani hapo. Wakipokea zawadi hiyo kwa niaba ya wengine ni Bi. Anjelina Masawe,(wa kwanza kushoto), Bi. Eliza David (wa pili kushoto) na Meneja wa baa hiyo Bw. Thadey Sebastian.

Shindano la Fanya Kweli Kiwanjani limefikia tamati kwa jiji la Dar es salaam huku wapenzi wa bia ya Tusker wakishuhudia baa ya Kinondoni M.K Pub ikiibuka kidedea baada ya kuzibwaga baa nyingine 9 zilizokuwa zinachuana kwenye shindano hilo.
Shamrashamra za kuipongeza baa hiyo zilipambwa na burudani ya muziki kutoka kwa ma Dj wa redio E-fm na watangazaji wa kituo hicho waliojumuika na mameneja wa bia ya Tusker kuipongeza baa hiyo.
Uchangamfu wa kiwanja hicho uliongezeka zaidi mishale ya saa moja jioni baada ya wadhamini wa shindano hilo kuanza kutoa zawadi kwa wateja wa bia ya Tusker waliofuruka kiwanjani hapo.
Kwa upande wake Bw. Francis Kimbona mteja wa siku zote kiwanjani hapo alitoa pongezi kwa wadhamini wa shindano hilo kwa kuanzisha kitu chenye lengo la kukuza zaidi mauzo ya baa mbalimbali za mitaa tunayoishi.
“Mashindano kama haya ni muhimu kwa kukuza kipato cha hizi baa zetu na niwaombe tu wadhamini waendelee kuonyesha mfano kwa jamii” aliongeza Bw. Kimbona.
Naye meneja wa bia ya Tusker Bi. Sialouise Shayo hakusita kuipongeza baa hiyo kwa kuibuka na ushindi huku akiwashukuru wateja wa bia hiyo kwa kuonesha uzalendo pale walipoombwa kuzipigia kura baa zote 50 zilizoorodheshwa kwenye shindano hilo.
“Tumepokea ushiriki mkubwa kutoka kwa wadau wakati wote wa shindano hili zaidi ya vile tulivyotarajia, hivyo nitoe tu pongezi kwa wateja wote wa bia ya Tusker walioshiriki katika kuzipigia kura baa za mitaa wanayoishi ili kuziwezesha zishinde shindano hili.” aliongeza Bi Shayo.
Kampeni hiyo ambayo imedumu kwa takriban muda wa wiki tano imekua na lengo la kuziibua baa mbalimbali za mitaa tunayoishi na kuzitangaza kwa wadau wa kinywaji cha Tusker ambapo wadau hao walipewa jukumu la kushiriki kuzipigia kura baa zetu pendwa ili zishinde shindano hilo.
Kupitia bia ya Tusker mameneja wa kinywaji hicho waliweza kuorodhesha baa 50 kwenye shindano hilo ambapo kwa muda wa wiki tano wa kampeni baa 10 zilipata kuchuana vikali kila wiki ili kuweza kumpata mshindi mmoja tu. Hivyo basi ndani ya wiki tano za shindano baa ambazo ziliibuka kidedea ni pamoja na;- “Toroka uje ya Kimara-Korogwe, Yenu bar ya Ubungo-Maji, New Jambo bar ya Mabibo, Kilwa road Pub ya Kurasini na “MK Pub ya Kinondoni iliyofunga shindano hilo.
Shindano hilo limefikia tamati kwa mkoa wa Dar es salaam huku mipango ya kulisogeza mikoani pia ikiendelea kuwekwa vizuri.
Kwa taarifa Zaidi tembelea;
Kurasa za facebook Tusker Tanzania na Twitter @Tusker Tanzania