BONGOCLAN Tanzania

Website yetu ipo katikamatengenezo

Copyright © BongoClan Tanzania™ | Published By Gooyaabi Templates | Powered By Blogger
Design by WebSuccessAgency | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com

HABARI ZILIZOSOMWA SANA WIKI HII

Wema ni kweli anavuta Bangi???

Bw. Nickolas Mwaisaka (51) mkazi wa Kurasini na mpenzi wa bia ya Tusker akikumbushia enzi zake stejini baada ya kujumuika na wateja wengine wa bia ya Tusker kuipongeza baa ya wiki ya “Kilwa road Pub” iliyopo Kurasini jijini Dar es salaam. Baa hiyo iliibuka mshindi wa nne wa kampeni ya Fanyakweli Kiwanjani inayoendeshwa na Bia ya Tusker kutoka SBL.

Bi. Anjelina Urassa ambaye ni mpenzi wa bia ya Tusker akifurahia burudani ya muziki wakati wa sherehe za kuipongeza baa ya wiki ya “Kilwa road Pub” iliyopo Kurasini jijini Dar es salaam ambayo ilishinda na kuwa baa ya nne katika shindano la “Fanya Kweli Kiwanjani” linalodhaminiwa na bia ya Tusker.


Bw.Gadner G Habash (kulia) akimkabidhi Bi. Magret Mjata zawadi ya fulana, bia za bure na mfuko baada ya kujibu swali kwa ufasaha wakati wa hafla ya kuipongeza baa ya wiki ya “Kilwa road Pub” iliyopo Kurasini jijini Dar es salaam ambayo ilishinda kwenye Kampeni ya Fanyakweli Kiwanjani inayodhaminiwa na bia ya Tusker.

Mhudumu wa chapa Tusker toka SBL Bi. Veronica Mbilinyi akikabidhi zawadi ya mfuko wenye bia za bure kwa Bw. Michael James mkazi wa Kimara ambaye ni mpenzi wa bia ya Tusker aliyejumuika na marafiki kuipongeza baa ya wiki ya Kilwa road Pub iliyopo Kurasini jijini Dar es salaam baada ya baa hiyo kuibuka mshindi wa shindano la Fanya Kweli Kiwanjani linaloendeshwa na bia ya Tusker

Tarehe 06 Juni 2015 Dar es Salaam,
  
Kampeni ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani, imechukua sura nyingine wiki hii baada ya kumpata mshindi wa nne wa promosheni hiyo ambayo imebakisha muda wa wiki moja tu kufikia kikomo.
Sura hiyo imejidhihirisha siku ya jumamosi baada ya “Kilwa road pub” ya Kurasini kuibuka mshindi wa wiki wa shindano la Fanya kweli Kiwanjani linaloendeshwa na bia ya Tusker kutoka SBL.
Utaratibu wa utoaji zawadi kwa baa zilizoshinda umekua ni kuwafanyia promo za nguvu ambazo zinaambatana na zawadi za aina mbalilimbali kama vile;-bia za bure, fulana za bure na bangili za mkono kwa wateja
Hadi mishale ya saa moja jioni Kiwanja hicho kilikua kimechangamka vilivyo ambapo wapenzi mbalimbali wa kinywaji cha Tusker walifika kiwanjani hapo kufurahia burudani ya mziki uliokua ukipigwa na kusikika moja kwa moja toka redio E-fm.
Akiongea na waandishi wa habari waliofika kiwanjani hapo Meneja wa baa hiyo Bw. Napoleon Mwanjelwa alisema “Nimefurahi sana kwa kuwa ushindi huu umetuletea neema siku ya leo”. Akifananua zaidi Bw. Mwanjelwa aliongeza kuwa baa hiyo haijajahi kuuza bia kupita kiasi kama siku hiyo na kuwashukuru mameneja wa Tusker kuanzisha shindano lenye tija kwa baa za mitaa tunayoishi.
Akikabidhi zawadi ya fedha taslim kiasi cha Tsh 100,000/= kwa wahudumu wa baa hiyo baada ya kufanya kweli kwenye upande wa huduma kwa siku hiyo, Afisa mauzo wa SBL eneo la Kurasini Bi. Rahma Mjata alisema “Tunaipongeza Kilwa road Pub kwa kuibuka mshindi wetu wa wiki na zaidi niwashurkuru mashabiki walijitoa kuipigia kura baa hii”. Bi Mjata aliongeza kuwa baa hiyo imeshinda baada ya mashabiki zaidi ya 50 kuipigia kura kupitia njia mbalimbali za mitandao na pia kupitia kipindi cha Ubaoni kinachorushwa na redio E-fm.
“Hadi kufikia sasa baa zaidi ya 40 za hapa jijini zimeshindanishwa na kuibua washindi 4 ambao ni; Toroka Uje bar ya Kimara, Yenu Bar ya Ubungo, New Jambo Bar ya Mabibo na leo hii Kilwa road pub-Kurasini” alimalizia Bi. Mjata.