Tarehe 23 Mei 2015 Dar es Salaam, Shindano la
Tusker Fanyakweli Kiwanjani linaloendeshwa na Kampuni ya Bia ya Serengeti chini
ya udhamini wa bia yake ya Tusker limempata mshindi wa pili wa Kampeni hiyo
kiwanja cha “Yenu baa”. Baa hiyo maarufu inayopatikana maeneo ya Ubungo karibu
na Wizara ya Maji imeibuka kidedea mara baada ya kupigiwa kura na wapenzi wengi
wa bia ya Tusker kwa wiki iliyopita kupitia kipindi cha Ubaoni kinachorushwa na
redio E-fm.
Baa hiyo ilipigiwa kura mara baada ya kuorodheshwa
na Kampuni ya Bia ya Serengeti chini ya udhamini wa bia yake ya Tusker kwenye
shindano hilo ambapo baa nyingine 9 zilichuana vikali kumpata mshindi wa wiki.
Mapema siku ya jumamosi, Kampuni ya bia ya Serengeti
kwa udhamini wa bia yake ya Tusker ilifunga kambi maeneo ya Ubungo maji na
kuporomosha burudani ya nguvu kwa wapenzi wa bia ya Tusker waliofika kuipongeza
baa hiyo kwa ushindi walioupata.
Akiielezea baa hiyo kwa undani mara baada ya
kukabidhiwa zawadi ya tisheti na bia ya Tusker aliyojishindia wakati wa sherehe
ya kuipongeza baa hiyo, mmoja wa wapenzi wa bia hiyo aliyefika kwenye eneo la
tukio ambaye alifahamika kwa jina la Steven Mbele alisema...”Mimi nimeifahamu
baa hii tangu mwaka 1993 kipindi hicho nilikua nasoma chuo kikuu cha Dar es
salaam hapo mlimani na mara nyingi kila baada ya masomo mida ya jioni nilikua nakuja
hapa na marafiki zangu kukata kiu, hivyo ubora wa huduma za baa hii ni tokea
enzi za zile.” Bw. Mbele aliongeza kuwa amefurahishwa baada ya kusikia baa hiyo
imeibuka na ushindi na kuipongeza Kampuni ya bia ya Serengeti kuanzisha
shindano ambalo nia na madhumuni yake ni kuziinua baa za mitaa tunayoishi.
Washindi wengine waliojinyakulia zawadi mbalimbali
kama;- mifuko, Tisheti na bia za bure ni pamoja na Alex Minja, Steven Thadei na
Bi. Magret Mjema.
Akiongea na waandishi wa habari waliofika eneo hilo,
Meneja Mauzo wa SBL kanda ya Ubungo Bw. Victor Mhindi alisema “Tunaipongeza
“Yenu Baa” kwa kuwa mshindi wetu wa wiki nyinyi wenyewe ni mashahidi na mmejionea
huduma za hapa jinsi wahudumu walivyo chap chap na wanavyofanya kazi kwa
bidii”. Bw. Mhindi aliendelea kusema kuwa Kampuni ya bia ya Serengeti
inajivunia kutoa sapoti kwa viwanja mbalimbali vya mitaa tunayoishi na kuwasihi
wadau na wapenzi wa kinywaji cha Tusker kuendelea kuzipigia kura baa
zinazoendelea kuorodheshwa kwenye shindano la Fanyakweli Kiwanjani ili kupata
kilicho bora.
Naye Meneja wa baa hiyo Bw. Anselim Kimario ambaye hakusita
kuimwagia sifa Bia ya Tusker alisema kuwa amefurahia zawadi ya fedha taslimu
Tsh 100,000/= waliyopewa na mameneja wa Tusker baada ya kufanya kweli na
kuongeza kuwa ushindi wao kama baa ya wiki umeongeza mauzo ya baa hiyo
maradufu.
“Hiki ni kitu cha tofauti kwa kweli ninashukuru sana
na niwapongeze sana mameneja wa Tusker kwa kutuandalia pomosheni hii ya Fanyakweli
Kiwanjani kama mnavyoona baa yetu leo imechanganya kupita maelezo”.
Ili
kuiwezesha baa ya mtaa unaoishi tembelea baa hiyo kisha burudika na kinywaji
cha Tusker na piga picha nyingi uwezavyo na uipendekeze baa hiyo kwa kuweka
picha hizo kwenye kurasa za jamii (Facebook na Twitter) za Tusker au kusikiliza
kipindi cha Ubaoni kinachorushwa na redio E-fm kati ya saa tisa hadi moja usiku
ndani ya siku za juma kwa maelezo zaidi.