MCHEKESHAJI mahiri katika tasnia ya filamu Swahilihood Hemed Maliyaga
‘Mkwere Orijino’ amesema kuwa anaposema ukweli haogopi kurogwa kwa
sababu anaamini anachokisema ni kwa ajili ya kuweka sawa kama ni rafiki
au mwigizaji mwenzake akienda tofauti.
“Mimi nasema tu, siogopi kurogwa bwana utaniroga wewe mimi narogwa na
watanzania wengi ninaowafurahisha kila siku, nasema wasanii tubadilike
katika kujitenga katika matukio kama maradhi, misiba na sherehe
tushirikiane tupendane,”anasema Mkwere.
Mkwere alisema hayo wakati akiongelea suala la baadhi ya wasanii
kujitenga na wasanii wenzao kwa mitazamo ya kipato, au makundi makundi
ambayo kwake haoni kama yana nafasi katika maisha ya wasanii wa filamu
na komedi ambao siku ya siku wote ni kitu kimoja kwani hawana tofauti
sana kiubinadamu.