Bila shaka mnajua fika kwenye uchaguzi ujao october CCM itaendelea
kutawala kama kawaida na hii ni kutokana na sababu nyingi tuu ..leo
nitaeleza tano tuu na pia nitaeleza sababu tano zitakacho kifanya chama
cha ACT kuwa chama kikuu cha Upinzani Tanzani...
Moja ya sababu inayoifanya CCM kuendelea kutawala ni kuwa na
hazina ya wapiga kura..huu ni ukweli ulio wazi maana wapiga kura walio
wengi ni wakina mama na wakina baba na hawa wengi ni CCM na hata
ukichukulia mfano kwenye zoezi ili linalo endelea la uandikishaji wa
wapiga kura utagundua kuwa walio hotokeza wengi ni wakina mama na wakina
baba ambao wengi ni wapiga kura wa kudumu wa CCM..wapiga kura wa
chadema wao wamejaa kwenye mitandao lakini huwa hawaendi kujiandikisha
na hawana sifa ya kupiga kura hii huwapa ushindi wa mezani CCM kila leo.
Pili CCM wanajua kutatua migogoro inayo jitokeza bila kuleta
madhara ukilinganisha na vyama vya upinzani hasa Chadema na UKAWA..mtu
anaweza kujidanganya muda huu kuwa CCM imevurugika oooh CCM kuna makundi
na yatakimaliza lakini mkitaka kuhakikisha kuwa CCM itatawala milele na
inajua kumaliza makundi subiri muone wakati wakuelekea uchaguzi mkuu
ndio hapo kila mtu ataamini kuwa hiki chama kita tawala milele na kama
mtakumbuka kipindi kilicho pita kabla ya Jk kulijitokeza makundi mengi
lakini yalikwisha na CCM ikasonga mbele wakiwa wamoja...tofauti na UKAWA
hasa Chadema hawana uwezo wa kuhimili vishindo vya makundi bila kuleta
madhara na mkitaka kuamini subirini wakati wa kumpata wagombea
mbalimbali kuputia UKAWA hasa mgombea Urais hapo ndio mtaamini UKAWA
hawana uwezo wa kuhimili makundi na watasambaratika au watakwenda wakiwa
wamegawanyika kabisa na ndio maana hadi sasa hakuna anaye onesha nia ya
kugombea hasa Urais maana wanajuana walivyo(patachimbika)
Tatu CCM wana hazina ya viongozi ambayo ni ndefu kwa hiyo wana
uwezo wa kuuwa makundi kwa kuwaacha wote walio kwenye makundi na
kuchagua mtu ambaye hatoki kwenye makundi na wakaendelea kutawala
milele...maana njia pekee ya kuuwa makundi ni kujichinjilia mbali wote
walio kwenye makundi na kuchukua mtu tofauti na wote wata tulia maana
kila mmoja kakosa..lakini huko UKAWA safu ni nyembamba saba kiasi kwamba
ni vigumu kuchagua nje ya makundi hasimu..mfano UKAWA kuna kundi la
Slaa , na Lipumba..ukiwatoa hawa hakuna mwingine mwenye sifa au anaye
weza kugombea kiti cha Urais sasa kazi inakuja jinsi ya kuunganisha haya
makundi bila kuleta mpasuko ni ngumu maana nje ya hao hakuna na
ukipendekweza mmoja kati ya hao bado kutakuwa na mpasuko na hapo ndio
mtakubaliana nami kuwa CCM itatawala milele..
Nne CCM ina umoja wa vijana ambao ni hazina,hai na wenye
nguvu...hapa pia ndipo CCM inapo tofautiana sana na UKAWA ambao wamejaza
vijana wengi lakini ni wapiga kelele tuu na wengi wao kujiandikisha
hawaendi na hawana sifa za kupiga kura halafu wengi wao wana nunulika
kirahisi..kwa mfano ukiangalia Bavicha ni kama imekufa kabisa tota
aondoke Heche imekufa kabisa kazi zote zina fanywa na wazee ..Bavicha
wameponzwa na makundi ya kugombea uenyekiti na ndio yanao utafuna umoja
huo kiasi kambwa mwenye kiti wao ana kosa ushirikiano na anashindwa
kuwaunganisha vijana.. Bavicha wengi wanacho fahamu ni kuongea kama
Mbowe tuu ...pia huu ni ushahidi CCM kutawala milele..
Tano CCM wanajua jinsi ya kujipanga na kukabili yanayo wakumba
hasa maswala ya ufisadi wa baadhi ya wanachama na huja na suluhu ndio
maana hata wakienda kwa wananchi huwa sikiliza lakini tofauti na UKAWA
hasa chadema huwa hawana majibu zaidi ya kuadithia story za ufisadi na
hawana lingine la kuwambia wananchi zaidi ya story za ufisadi na ni
waongeaji sana kuliko vitendo hivyo hilo linawafanya wananchi wawachoke
na waonekanae hata wakipewa nchi nao watakula tuu!
Pia kuna sababu tano zitakacho kifanya chama cha ACT kuwa chama kikuu upinzani kuanzia October...
Kwanza ACT kinatangazwa sana na kupewa airtime na vijana wa chadema
kiasi kwamba kila mtu anataka kukifahamu na watu wametamani sana
kujiunga na hiki chama kipya ambacho kina isumbua chadeema kiasi hiki
hadi wana sahau mambo yao..
ACT kitapata majimbo mengi hasa ya upinzani hasa ya chadema kutokana na
nguvu aliyo nayo bwana Zitto kabwe na hivyo atawashawishi sana wananchi
na watakichagua maana kila mtu anajua nguvu ya Zitto kwa wananchi hata
UKAWA wana fahamu hilo.
ACT itakuwa kimbilio la vijana wengi kutokana na nguvu ya Zitto na bila
shaka hili halina ubishi kwa kuwa ni wazi kuwa Vijana wengi walio
chadema wamepwnda siasa na wameipenda Chadema kupitia Zitto na
walivutiwa na Zitto kutokana na uwezo wake mkubwa katika siasa hivyo
wengi watajiunga nae na hapo Chadema hawato amini bali wajiandae sana
kwa upinzani mkubwa...wabunge wengi vijana wa chadema wamepata ubunge
kwa kupitia nguvu ya Zitto na hilo hawawezi kubisha.
Tatu ACT imepata mtu mwenye ushawishi mkubwa na mwenye uwezo wa kujenga
hoja kuliko kiongozi yeyote yule wa upinzani..Zitto ni mtu aliye
barikiwa nguvu ya ushawishi kabisa kila mtu anajua anapo simama
kuongelea jambo kila humvuta kila mtu bila kujali itikadi yake
...tofauti na kule chadema ambapo wote wameigana jaziba hakuna anaye
weza kuongea jambo bila jaziba au munkari hili litakifanya chama cha ACT
kuwa chama kikuu cha upinzani..
Nne ACT imepata pakujifunza maana wameona wenzao hasa chadema walipo
kwama hasa uwezo mdogo wa kushawishi watu kuwapigia kura....maana
chadema hawana njia nyingine ya kushawishi watu zaidi ya kusema ufisadi
na hii imewachosha watu maana watu wanajua hata wao si wasafi lakini kwa
timu ya ACT hakika kutakuwa na suluhu hivyo chadema wata sahaulika.
Mwisho ACT kitajengwa sana na walio kosa haki zao chadema hivyo wataona
ni sehemu ya kukimbilia ..pia wabunge wengi au vijana watakao kosa
nafasi kutokana na mfumo wa chadema wa kuwapata viongozi au wabunge
ambao hautoi haki ACT itakuwa kimbilio lao!
Karibuni wana jamvi..
#zamuyakokijanakajiandikishe
By Ruttashobolwa