Na Musa Mateja/Ijumaa Wikienda
WAKATI mama mzazi wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond
Platnumz’, Sanura Kasim ‘Sandra’ akiwa nchini India kwa matibabu ya
tatizo la kiafya linalodaiwa kuwa ni kupooza, hapa Bongo dalili za
Diamond na mpenzi wake wa sasa, Zarinah Hassan ‘Zari’ au The Boss Lady
kufunga ndoa zinanukia.......
Chanzo makini kimeliambia Ijumaa Wikienda kwamba, licha ya mama Diamond
kupelekwa India Januari 27, mwaka huu na msafara wa watu wawili, nyuma,
Zari alitua Bongo tangu Januari 30, mwaka huu lengo kubwa likiwa
kumuuguza mama mkwe wake huyo.
Unaweza Soma : Vazi hili la Lulu lazua mzozo mtandaoni, hivi ndo alivyokua kavaa. Cheki picha hapa
ATUA DAR, AENDA SINZA-MORI
Chanzo kikazidi kuweka wazi kuwa mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Diamond alimpokea na
kwenda naye nyumbani kwake, Sinza-Mori jijini Dar bila kumwambia kama
mama yake amepelekwa India kwa matibabu.
“Diamond alikwenda kumpokea Zari lakini hakumwambia kama mama yake
amekimbizwa India kwa matibabu na yeye (Zari) alikuja kwa lengo la
kumuuguza mama mkwe wake,” kilisema chanzo.
BAADA YA KUMKOSA MAMA MKWE
Habari zaidi zilisema kuwa, walipofika nyumbani na Zari kuambiwa mama
Diamond amepelekwa India, aliumia sana na kumlaumu mpenzi wake huyo kwa
nini hakumwambia kuhusu safari ya mama tangu walipokutana uwanja wa
ndege.
Unaweza Soma : Picha za kilichojiri katika utengenezaji wa video mpya ya Linex na Diamond hizi hapa
YAISHA, DIAMOND AMPELEKA ZARI KWENYE UJENZI
Baada ya kuwekana sawa kuhusu usiri wa safari ya mama’ke, Diamond
alimchukua Zari na kumpeleka kwenye nyumba yake anayoijenga Mbezi-Beach,
Dar kwa lengo la kumuonesha sehemu ya mali zake ambapo ilisemekana
nyota huyo wa Uganda aliipenda ramani ya nyumba hiyo.
ZARI AGOMA TENA KULALA HOTELINI
Katika siku za hivi karibuni, tuliwahi kuandika kuwa Zari alilala kwa
mama Diamond, akapika na kupakua ambapo mawifi zake walimsifia.
Hata katika ujio wake wa Juni 30, mwaka huu, mrembo huyo mwenye utajiri
mkubwa aligoma kwenda kulala hotelini na kumwambia Diamond atalala naye
nyumbani kwao, Sinza-Mori.
Unaweza Soma : DIAMOND AMTUSI VIBAYA MPENZI WA ZAMANI WA ZARI, KING LAWRENC
ZARI AANZA KUBADILI DINI?
Zari ni Mkristo wa Kanisa la Born Again ambalo ni la kiroho nchini
Uganda. Aliingia kwenye imani hiyo baada kuokoka na kubatizwa kwa maji
mengi kama Biblia inavyotaka lakini kwa kuwa na Diamond kuna dalili za
kuanza kubadili imani ili kutimiza mipango ya ndoa.
“Ukiachia kwenda kwenye nyumba hiyo ya Mbezi pia Diamond ameshaanza
kumfundisha Zari baadhi ya mambo ya kidini,” kilisema chanzo.
IJUMAA ATINGA BAIBUI
Ijumaa iliyopita ambayo kiimani, Diamond hupenda kuvaa mavazi ya Kiarabu
ambayo hutafsirika ni ya Kiislam, Zari naye alitupia vazi la baibui ili
kwenda sawasawa na mwandani wake huyo.
Unaweza Soma : LE MUTUZI AMLIPUA HUYU MDADA ANAYE TUKANA WATU KWENYE MITANDAO
WAENDA SONGEA WOTE
Wakati Ijumaa Wikienda likijiandaa kwenda mitamboni, habari za moto ni
safari ya Diamond kwenda mjini Songea ambapo ni makao makuu ya Mkoa wa
Ruvuma.
Diamond alikwenda kwa ajili ya shoo ya sherehe za Chama cha Mapinduzi
(CCM) kutimiza miaka 38 tangu kuasisiwa kwake. Sherehe hizo zilifanyika
kwenye Uwanja wa Majimaji jana.
ZARI KWAPANI
Habari za uhakika ni kwamba, katika safari hiyo, Diamond alimuweka Zari kwapani na kwenda naye kwa lengo la kumpa kampani.
DIAMOND: KILA KITU KINA WAKATI WAKE
Ijumaa Wikienda lilimtafuta Diamond kwa njia ya simu ambapo awali
alikiri mama yake kupelekwa India kwa matibabu. Kuhusu Zari kubadili
dini, kuvaa hijabu na kufunga ndoa, alisema: “Mbona mna maswali sana
jamani, kila kitu kina wakati wake.”
Unaweza Soma : Diamond Alipwa Millioni 50 Cash Kuwatumbuiza CCM Leo