Kwa mujibuwa mtandao wa JF, Mwigizaji wa vichekesho Lucas Mhuvile,
almaarufu kama Joti, anayepiga kazi kwenye kampuni ya Orijino Komedi,
amemvisha pete mpenzi wake wa siku nyingi, ikiwa ni ishara na dalili
njema kwamba safari ya kuelekea kwenye taasisi muhimu zaidi duniani ya
NDOA imewadia..
Akiwa na swahiba wake wa siku nyingi, Mr. Mjuni Sylvatory a.k.a
Mpoki, Joti alionekana mwenye furaha muda wote kwa kutimiza tendo hilo
huku akiwa amealika watu wachache sana kuhudhuria tukio hilo. ni taarifa
za juuju. Kama ni kweli, tunampongeza sana na kumtakia kila la kheri
yeye pamoja na mwenza wake