Dully Sykes amedai kushangazwa kusikia watu wazima kama TID na Q Chillah
wakilumbana kwa jambo la miaka mingi iliyopita na kwamba mambo kama
hayo wanapaswa kuwaachia wadogo zao mathalan Alikiba na Diamond.
Dully ameiambia Bongo5 kuwa TID na Q wamemfedhehesha.
“Hawa ni watu wazima,” amesema Dully. “Mimi kama kuwazungumzia
ninawazungumzia Diamond na Alikiba. Hawa ni vijana, kwanini Q Chillah na
TID wasimalize masuala yao? Wanashindwa kuweka pembeni tofauti zao!
Kwanini wanagombana wakati ni watu wazima tayari?
“Sishangai ugomvi wa Alikiba na Diamond nashangaa ugomvi wa TID na Q
Chillah kwasababu Diamond na Alikiba ni watoto! Mimi nitashangaa TID
kugombana na Q Chillah kwasababu wao ni watu wazima. Wanatakiwa wapatane
ili watoto kama Diamond na Alikiba wapatane. Mimi siwezi kuzungumza nao
chochote waache wagombane.”