Diamond Platnumz ni miongoni mwa marafiki wa karibu wa msanii Dully
Sykes ambaye weekend iliyopita alimpoteza baba yake mzazi Ebby Sykes,
lakini hakuweza kuhudhuria msiba huo kutokana na sababu ambazo amezitoa
leo.
Diamond ambaye wakati msiba huo unatokea alikuwa Zanzibar na mpenzi wake
Zari, ameelezea sababu zilizomfanya kushindwa kuhudhuria mazishi.
“Watu waliniona niko zanzibar lakini walikuwa hawajui nimeenda kufanya nini,” Diamond
ameiambia 255 ya XXL ya Clouds FM. “Usiangalie kila unachokiona Instagram ukajua mtu labda kwasababu alikuwa anafanya starehe.
Niko katika kipindi ambacho sio kizuri kwangu mimi na familia yangu
kwasababu kuna vitu ambavyo siwezi kuvizungumza lakini, na siwezi
kuviweka kwenye media ndo maana watu wengine wanaweza kuniona nacheka
lakini […kwanza mama yangu anaumwa na anaumwa sana sijawahi kulizungumza
hili ndo nalizungumza hapa, hapa ninapoongea na wewe yupo India, kuna
vitu vingi vinaendelea, siwezi kusema nilikuwa Zanzibar nafanya nini