BONGOCLAN Tanzania

Website yetu ipo katikamatengenezo

Copyright © BongoClan Tanzania™ | Published By Gooyaabi Templates | Powered By Blogger
Design by WebSuccessAgency | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com

HABARI ZILIZOSOMWA SANA WIKI HII

Wema ni kweli anavuta Bangi???


TAARIFA KWA UMMA
BENKI YA I&M YAZINDUA HUDUMA YA KWANZA YA MFUMO WA KIELEKTRONIKI YA MASAA 24 KATIKA JENGO LA VIVA TOWERS, POSTA JIJINI DAR ES SALAAM
Jumanne 03/02/2015: I&M Bank (T) Limited imeendelea kuonyesha muelekeo mzuri katika soko baada ya kuzindua huduma ya kwanza na ya kipekee ya ya kibenki ijulikanayo kama “Banking lounge” itakayokuwa ikifanya kazi kwa masaa 24 kwa siku saba, ndani ya ghorofa ya kwanza katika jengo la Viva Towers, moja kati ya maeneo muhimu jijini Dar es salaam. Tanzania.

Hili ni jaribio la kipekee kwa Benki hiyo, kutoa huduma mbalimbali za kibenki kama vile;-Mashine ya kubadilisha fedha za kigeni, mashine ya mfumo wa ATM ya kuweka na kutoa fedha, “Siku yoyote, muda wowote” ndani ya masaa 24 katika siku saba za wiki.

MASHINE YA KUBADILISHA FEDHA ZA KIGENI: Ni sehemu ya kubadilishia fedha itakayokuwa ikifanya kazi kwa muda wa masaa 24 ndani ya siku saba za wiki. Hii itamuwezesha mteja kubadilisha fedha zake za kigeni na kupokea shilingi ya kitanzania bila ya kuwa na mtoa huduma. Hii itakuwa na umuhimu zaidi kwa wateja ambao watapenda kufanya miamala yao hasa nyakati za jioni/usiku huku kukiwa hakuna haja ya mteja kuwa na akaunti ya benki hiyo pindi anapotaka kupata huduma hii bali anachohitaji ni pasipoti halali ili kupata huduma.

MASHINE YA KUWEKEA FEDHA: Itamsaidia mteja kupata huduma kwa masaa 24 ndani ya siku saba hasa kwa maduka na biashara yanayofungwa mida ya jioni/usikuili kuweka fedha za mauzo yao ya siku nzima katika akaunti za benki zao muda wowote. Huduma hii ni ya kila siku ikiwemo siku ya jumapili na siku za sikukuu. Benki hii imefunga “kifaa maalum cha kuwekea fedha”, ambacho kiasi chochote kikubwa cha fedha kinaweza wekwa kwa usalama wa hali ya juu katika mashine hiyo pasipo na uhitaji wa mtoa huduma wa benki.
Mashine hii itahesabu fedha na itatoa risiti kwa mteja. Mashine hii ina kasi ya ajabu na uwezo mkubwa wa kuweka fedha nyingi, ikiwa na teknolojia ya hali ya juu kama vile kitambua fedha endapo itakua ni feki au la, kichambuzi na kitambuzi namba n.k.
MASHINE ZA ATM: Mashine za ATM zilizowezeshwa na VISA zitakazokuwa zikifanya kazi kwa masaa 24 zitawahudumia wateja na wa watumiaji wa kadi za VISA.
Zaidi ya huduma hizi za hali ya juu, Benki pia imeanzaisha “VIP SERVICE LOUNGE” ambayo inatoa huduma ya kibenki isiyo ya fedha, katika hali ya kisasa na starehe. Ikiwa na TV na mashine za kujipatia kahawa, mteja anaweza kukaa na kupumzika, katika hali salama, wakati wahudumu waliofunzwa kwa umahiri wakiendelea kumhudumia, kuanzaia saa 2 asubuhi mpaka saa 2 usiku. Pia wahudumu watasikiliza na kupokea mahitaji yote ya wateja yatakayotolewa huduma katika tawi letu la Maktaba kama vile:-maombi ya kufunguliwa akaunti, maombi ya TT/TISS, huduma za vitabu vya hundi, kadi za malipo ya kabla ya fedha za kigeni, huduma ya kadi za ATM, mikopo, maombi ya kadi za BPesa, taarifa nyingine za kibenki na msaada katika huduma nyingine za kibenki.
I&M imekuwa ni benki ya kwanza kuanzisha huduma hii ya teknolojia ya hali ya juu katika soko la Tanzania ambapo “Smart Banking Solutions Ltd” kwa mara nyingine tena imepiga hatua kwa kuungana na benki hiyo na kufunga mashine za kuweka na kutoa fedha sambamba na kubadilishia fedha za kigeni.” .

Akielezea faida za mfumo huu, Afisa mtendaji mkuu wa benki ya I&M  Bw. Anurag Dureha alisema “Kwa mfumo huu mpya mteja wa I&M sasa atakuwa na uwezo wa kutumia huduma za kibenki kwa urahisi”. Tawi hili jipya linampa mteja njia mbadala za kufanya miamala, zaidi ya ile ya awali kama vile matawi ya benki, intaneti na simu za mikononi.
“Kwa kuanza, fedha ya kigeni itakayobadilishwa na mashine hizi ni dola za kimarekani muda mfupi baadae tutaongeza fedha nyingine za kigeni ili kutimiza mahitaji ya wateja wetu wanaotoka sehemu mbalimbali duniani kote” aliongeza Bw. Dureha.


aaaa
Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya I&M, Anurag Doreha  (kushoto) akiongea na wadau wa benki hiyo hawapo pichani wakati wa uzinduzi wa tawi  na mfumo mpya wa kielektroniki uliovumbuliwa na Smart Banking Solutions Ltd ambapo mteja anaweza kuweka na kutoa pesa  sambamba na kupata huduma nyingine za kibenki kama kubadilisha fedha za kigeni kwa kutumia mashine za kielektroniki masaa 24 ya siku.Hafla hiyo ilifanyika Viva Tower-Posta jijini Dar es Salaam, Kulia ni Meneja wa I&M wa tawi hilo Bi. Shabina Manji.

Baadhi ya wadau wa benki ya I&M na waandishi wa habari wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mkuu wa benki hiyo Bw. Anurag Doreha , hayupo pichani wakati wa uzinduzi wa tawi jipya la kielektroniki , ambapo wateja wake wataweza kuweka na kutoa pesa kwa kutumia ATMs sambamba na huduma ya kubadili fedha za kigeni kwa masaa 24. Hafla hiyo ilifanyika katika tawi jipya la I&M, Viva Tower-Posta jijini Dar es Salaam. Benki hiyo imeungana na kampuni ya Smart Banking Solutions kuwaletea wateja wake huduma hii

Mkurugenzi Mkuu wa VIVA Tower Viral Manek, akikata utepe kama ishara ya uzinduzi wa tawi jipya la Benki ya I&M katika jengo hilo litakalotoa huduma masaa 24, kwa kuweka na kutoa fedha na kubadilisha fedha za kigeni kwa kutumia mfumo mpya wa mashine za kieletroniki (ATMs). Kushoto ni mkurugenzi mkuu wa benki hiyo, Bw. Anurag Doreha, Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya I&M, Anurag Doreha (katikati) akifafanua jambo baada ya uzinduzi wa tawi jipya la benki hiyo kufanyika katika jengo la Viva Tower ambapo huduma za kuweka, kutoa na kubadilisha fedha za kigeni zitakua zikifanyika masaa 24 kutumia mashine za kielektroniki(ATMs) kulia ni Mkurugenzi mkuu wa VIVA Tower Viral Manek na kushoto ni Meneja Masoko wa Smart Banking Solutions Limited, Salil Abbas Sadik. Hafla ya uzinduzi huo ilifanyika Viva Tower-Posta jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi mkuu wa VIVA Tower Viral Manek, akionesha kwa vitendo jinsi ya kuweka fedha katika moja ya mashine za kielektroniki ndani ya tawi jipya lililozinduliwa la benki ya I&M ikishirikiana na Smart Banking Solutions-Viva Tower-Posta jijini Dar es salaam ambapo mteja anaweza kuweka na kutoa fedha masaa 24 sambamba na kupata huduma ya kubadilisha fedha za kigeni kwa kutumia mashine za kielektroniki(ATMs).

Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya I&M, Anurag Doreha akiwaonyesha waandishi wa habari moja ya mashine inayotumika kubadili fedha za kigeni, baada ya kuzindua tawi jipya la benki hiyo maalum kwa shughuli za kuweka na kutoa fedha kwa kutumia mfumo mpya wa kielektroniki kupitia mashine za (ATMs). Hafla hiyo ilifanyika katika jengo la Viva Tower-Posta jijini Dar es Salaam ambapo benki hiyo imeshirikiana na kampuni ya Smart Banking Solutions Ltd.


Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya I&M, Anurag Doreha akionyesha mfano wa kutoa fedha katika moja ya mashine inayotumika kubadili fedha za kigeni. Mare baada ya kuzindua tawi na mfumo mpya ulioanzishwa na Smart Banking Solutions wa kuweka na kutoa fedha kupitia ATMs sambamba na kubadili fedha za kigeni ambapo mteja atapata huduma hii ndani ya masaa 24 ya siku. Hafla hiyo ilifanyika Viva Tower-Posta jijini Dar.


Meneja Masoko wa Smart Banking Solutions Limited  Bw. Salil Abbas Sadik akiwaeleza waandishi wa habari kwa undani jinsi mfumo huo  wa kielektroniki unavyofanya kazi ambapo mteja anaweza kuweka na kutoa fedha kupitia mashine za (ATMs) sambamba na kubadili fedha za kigeni masaa 24. Smart Banking solutions Ltd ndio waanzilishi wa teknolojia hiyo ambayo bado haijatumiwa na benki nyingine yeyote. Hafla hiyo ilifanyika Viva Tower-Posta jijini Dar.