Hivi karibuni kupitia kipindi cha Siz Kitaa cha Clouds TV, Q-Chief
alidai kuwa sababu za kujiondoa kwenye bendi ya TID, Top Band ni baada
ya muimbaji huyo wa ‘Zeze’ kumdhulumu mamilioni ya shilingi kutoka
kwenye album ya bendi hiyo.
Hata hivyo TID akiongea kwenye kipindi hicho hicho, amedai kuwa hiyo si
sababu sahihi na kwamba Chilla alikuwa na tamaa. TID amedai kuwa
kimsingi fedha hizo zilikuwa zake zaidi kwa kuwa ni yeye ndiye
aliyeandika nyimbo za album hiyo, kutoa jina na pia ni yeye ndiye
aliyefikia makubaliano na mhindi kuhusu kuiuza album hiyo.
Amedai kuwa baada ya kulipwa fedha hizo walikuwa wamekubaliana kuwa
zingetumika kununulia vyombo vya bendi. Pia alidai Q-Chief alilipwa
fedha kadhaa ambazo aliishia kuzilia bata na zilipokwisha aliamua
kuchukua polisi kumwendea TID kuwa amemdhulumu fedha yake.