Familia ya Mbasha inaendelea kutengeneza vichwa vya habari.
Baada ya mchungaji maarufu nchini, Gwajima kukanusha kuwa si baba wa
mtoto wa Flora Mbasha, mume wa muimbaji huyo wa muziki wa injili,
Emmanuel naye
amesema hatambui chochote kuhusu kuzaliwa kwa mtoto huyo.
Mbasha ambaye pia ni muimbaji wa muziki huo amesema ana mtoto mmoja
mwenye umri wa miaka kumi na kwamba taarifa za kuwa Flora amejifungua
anazisikia kama watu wengine.
“Nina mtoto mmoja, nina mtoto mmoja anaitwa Lizy na kama miaka 10 hivi.
Wewe ndo unanieleza mimi kama amejifungua, kama amejifungua ni jambo
jema na jambo la kumshukuru Mungu,” Mbasha alikiambia kipindi cha
Sunrice cha Times FM.
Kazi ipo hapo !