Nimejaribu kukaa na kutafakari matusi anayopewa Diamond na team Wema,
kisha katika pitapita zangu nikakutana na hili jamaa linajiita King
Lawrence (Lawrence Muyanga). Huyu jamaa nadhani amekuwa mtumwa wa
kufuatilia mienendo ya Diamond na Zari, kwani karibu kila tukio
analirusha huko instagram kwake.
Kwa namna anavyoaandika maneno ya kejeli hakuna shaka kwamba huyu jamaa
penzi la Chibu na Madam Zari limempiga za chemba vibaya mno. Jamaa kama
kapanic hivi hadi kakosa direction. Anataka kutengeneza kaushindani ka
kijinga na Chibu halafu Chibu mwenyewe kampotezea. Pamoja na kuwa jamaa
anaonekana change zipo ila hili la Chibu na Dangote pesa imeshindwa
kufanya kazi.