BONGOCLAN Tanzania

Website yetu ipo katikamatengenezo

Copyright © BongoClan Tanzania™ | Published By Gooyaabi Templates | Powered By Blogger
Design by WebSuccessAgency | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com

HABARI ZILIZOSOMWA SANA WIKI HII

Wema ni kweli anavuta Bangi???

Kume kuwa na stori kibao tangu Wema sepetu kuachana na Diamond platnumz,lakini kilicho make head lines zaidi ni hii ya Wema Sepetu kumfungulia Diamond mashtaka ya kumdai.

Kwenye interview aliyo ifanya baada ya kuzagaa kwa taarifa hizo za kufungua mashtaka kwaajili ya kumstaki mpenzi wake wa zamani,wema hapa anafunguka....
Kwenye Exclusive Interview, Wema Sepetu amesema haya;

“Taarifa hii imenishtua sana maana asubuhi ya jana nimekuta kwenye gazeti wameandika nikashangaa yaani hapa nimekaa kwa sababu muda mwingi siendeshi mimi akaunti yangu ya twitter, anaiendesha mtu wangu wa blog Bestizo maana nilikua nataka kutoa tamko“-- Wema Sepetu.

“Nilishasema ukurasa huu tulishaufunga na nilishasema haiwezi kujirudia tena, nashangaa watu wanarudi na maneno yale yale maana nimekaa kimya kwa kila kitu ili kuepuka haya maneno“

“Hakuna kitu ambacho namdai Diamond,hakuna siku hata moja nimefikiria kwenda kumshtaki Diamond labda kama kungekuwa kuna kitu chochote, yaani labda kungekuwa na ukweli wa kitu chochote siwezi kupoteza muda wangu kwenda polisi, sijawahi kufanya kitu cha namna hii hizi taarifa zimenishtua sana“



“Sijawahi kujiunga VICOBA maana sivijui, nilikua nimekaa na mtu akanambia labda Wemahujui hawa watu wa VICOBA wanajaribu kujitangaza kwa njia hii na kutengeneza hii kitu kwamba VICOBA wanaweza kukopa hadi Milioni kumi… kwanza mimi siwezi kukopa Milioni 10..“– Wema Sepetu.