BONGOCLAN Tanzania

Website yetu ipo katikamatengenezo

Copyright © BongoClan Tanzania™ | Published By Gooyaabi Templates | Powered By Blogger
Design by WebSuccessAgency | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com

HABARI ZILIZOSOMWA SANA WIKI HII

Wema ni kweli anavuta Bangi???



SERENGETI BREWERIES LTD
                         TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Shinyanga, Tanzania-Septemba 12/2014
BAADA ya kufanya maonyesho ya kuvutia katika zaidi ya mikoa sita nchini, shughuli hiyo ya Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) bado kabisa haijamalizika, na sasa macho yote yameelekezwa kwa wakazi wa Shinyanga ambao wanasubiri kwa hamu kubwa  kufahamu nini watapata kutoka Serengeti fiesta leo.
­­­­­­­­­­­­­­­­­­­
Upo uchangamfu wa aina yake kwa mashabiki wa hapa; kwa hakika karibu wakazi wote tuliokutana nao wamekwishajiandaa kuhudhuria shoo hiyo mbali na ukweli kuwa Serengeti Fiesta imekuja mkoani humu kwa kuchelewa kuliko ilivyotarajiwa. Onyesho la Serengeti Fiesta mjini Shinyanga lilipaswa kufanyika Septemba 6 mwaka huu kwenye Uwanja wa Kambarage, lakini likaahirishwa kutokana na ajali mbaya iliyotokea mkoani Mara ikihusisha magari matatu.

Wakazi wengi wa Shinyanga wamefurahia na kuipongeza timu nzima ya SBL kwa kujitolea kushirikiana na jamii wakati wa ajali hiyo iliyoua karibu watu 40, na kuzitaka kampuni nyingine kuiga mfano huo.

Timu ya SBL pamoja na wasanii waliwatembelea majeruhi hospitalini na kuzifariji familia zilizopoteza wapendwa wao, ambapo walichangia chakula na vitu vingine muhimu.

Katika kuonyesha kuwa SBL ipo nyuma ya kaulimbiu ya mwaka huu ya Serengeti Fiesta isemayo; ‘SambazaUpendo’, mapato ya mlangoni kwenye onyesho la Serengeti Fiesta 2014 mjini Musoma, yalipelekwa kwa familia zilizoathirika na janga lile la ajali.

Young Killa, Fid Q na Stamina wakiongozana na zaidi ya wasanii wengine 10 wenye vipaji vya hali ya juu, wameahidi kufanya onyesho la nguvu kwenye Uwanja wa Kambarage. Orodha ya wanamuziki hawa inawajumuisha pia akina Ommy Dimpoz, Linah, Recho, Ney wa Mitego, Chege na Temba, Nikki II, Mo Music na Kadja, ambao watasindikizwa na wasanii wenyeji wa mkoa wa Shinyanga.
Wakati maandalizi yakipamba moto, tulikutana na Meneja wa Kinywaji cha Serengeti, Bw. Rugambo Rodney, aliyekuwa na machache ya kuwaambia wakazi wa Shinyanga: “tiketi zipo tayari na maandalizi yanaendelea, ningependa kuwatia moyo wanaShinyanga, wahudhurie kwa wingi kwani tuna akiba ya vitu vingi na mambo makubwa kwa ajili yao.”
Baada ya Shinyanga, Serengeti Fiesta 2014 itakuwa njiani kuelekea Geita ikiwa ni mwendelezo wa maonyesho 18 yaliyoahidiwa kwa mashabiki.

About Serengeti Breweries Limited 
Serengeti Breweries Limited engages in the brewing, manufacturing, marketing and selling drinks made of malt, hops and barley and sorghum in Tanzania.
 Headquartered in Dar es Salaam, SBL brands include:- Serengeti Premium Lager, Serengeti Platinum, Tusker Lager, Tusker Lite, Kibo Gold, Uhuru Peak Lager, Pilsner Lager, Senator, The Kick and Guinness®.
 SBL is also the sole distributor of several international renowned spirits including Smirnoff Vodka®, Johnnie Walker®, Bailey’s Irish Cream ®, Richot®, Bond 7 Whiskey® and Gilbeys Gin®.
 Serengeti Breweries Limited is a subsidiary of East African Breweries Limited/ DIAGEO PLC.