Usiku wa Jumamosi ya Tarehe 30.Augost 2014, majira ya saa 10 alfajiri, Mwanamuziki nyota wa Bongo Flava Nasib Abdul 'Diamond Platnumz' alijikuta katika hali ya hatari hadi kuokolewa na Polisi mjini Stuttgart, Ujerumani, baada ya washabiki waliokuwa na hasira kuchoka kusubiri show.
Washabiki hao waliokuwa wamelipa ticket euro 25 kwa kiingilio
waliahidiwa kuwa show ingeanza saa 4.00 usiku, lakini walijikuta
wakisubiri hadi majira ya saa 10 usiku au alfajiri ndipo mwanamuziki
Diamond alipoletwa jukwaani na promota wake Mr.Awin Williams Akipomiemie raia wa Nigeria anajiita kama Britts Event.
Hapo ndipo washabiki hao walipoona kuwa hawakutendewa haki walianza
kurusha chupa na kutaka kumvamia mwanamuziki Diamond na promota wake.
Kilichowakera zaidi mashabiki ni pamoja na vyombo vibovu
vilivyofungwa katika ukumbi huo kitu ambacho kiliwafanya mashabiki
kuvunja vyombo vya muziki ma-Djs walishambuliwa na wapo hosptalini kwa
sasa.
Moja wa Djs hao alipoteza Lap top yake, mwanadada DJ Flor alipatwa
mstuko wa moyo na kukimbizwa hosptali, washabiki hao walimpa kipigo DJ
Drazee naye yupo hoi hospatal.
Polisi nchini Ujerumani wamesema tukio hilo la aibu halijawahi
kutokea, kwani msanii kuchelewa kufika jukwaani kwa ujerumani ni kitu
cha hatari sana kwani mashabiki wa ujerumani wanaheshimu sana muda wao.
Mpaka sasa polisi wanamsaka mwandaaji wa onyesho hilo na wamesema
kuwa wanachunguza thamani ya hasara iliyosababishwa na ghasia hizo na
pia itamfungulia mashataka promoter huyo raia wa Nigeria,ambaye pia
anachunguzwa kwa kusemekana anajihusisha na mtandao fulani wa biashara.
Kupitia Instagram Diamond alidai kusikitishwa na tukio hilo.
Kiukweli nimesikitishwa sana na uandaaji wa kampuni hii ya BRITTS EVENTS iliyoandaa show ya Stuttgart Germany… kinachoniuma na kunisikitisha zaidi ni jins watu walivyoamua kujitolea kuja kwa wingi kutusupport vijana wao, halaf mwisho wa siku promoter anatupeleka wasanii kwenye show saa kumi alfajiri… najua ni kiasi gani mmeumia na kuwa disappointed… lakini naomba mtambue kuwa halikuwa ni kosa langu, coz mimi ni mgeni tu, na nafata maelekezo ya promoter…hivyo nisingeweza kujiamulia kuja muda ninaoutaka mimi….
Kupitia Instagram Diamond alidai kusikitishwa na tukio hilo.
Kiukweli nimesikitishwa sana na uandaaji wa kampuni hii ya BRITTS EVENTS iliyoandaa show ya Stuttgart Germany… kinachoniuma na kunisikitisha zaidi ni jins watu walivyoamua kujitolea kuja kwa wingi kutusupport vijana wao, halaf mwisho wa siku promoter anatupeleka wasanii kwenye show saa kumi alfajiri… najua ni kiasi gani mmeumia na kuwa disappointed… lakini naomba mtambue kuwa halikuwa ni kosa langu, coz mimi ni mgeni tu, na nafata maelekezo ya promoter…hivyo nisingeweza kujiamulia kuja muda ninaoutaka mimi….