BONGOCLAN Tanzania

Website yetu ipo katikamatengenezo

Copyright © BongoClan Tanzania™ | Published By Gooyaabi Templates | Powered By Blogger
Design by WebSuccessAgency | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com

HABARI ZILIZOSOMWA SANA WIKI HII

Wema ni kweli anavuta Bangi???

Rapper mdogo kuliko wote Tanzania "Dogo D" mwenye umeri chini ya miaka 15 kutoka Mwanza ameachia wimbo unaowadiss wasanii kibao wakubwa wasanii wa mwanza Mo Music na Yong Killer lakini pia hakuwaacha wasanii wengine kama Nay wa Mitego, Dogo Janja, Pnc na wengineo
Ngoma hiyo aliyoipa jina la "Wamenichokoza" akiwa amemshirikisha King Silver amemdiss Mo Music na Nay wa Mitego kwa kusema 
"mwanzoni ulipokwenda pamoja tulikwenda kuhit basi nenda, kufanya ngoma yangu ndio unanipiga kalenda
wamitego acha poz kama dem, kama kidume kweli kwanini hupokei simu. 
hakuishia hapo aliendelea na kumdiss Young Killer  na Dogo Janja kwa kusema 

"Hakuna baba mwenye gari kuna baba mwenye nyumba, msodoki acha uongo kusema umejenge nyumba"....Dogo janjaro chunga utapauka utadhani goti la mbuzi wakati kwa madee unakula na kunywa nkujamba tu ushuzi"
alipofikia kumdiss msanii Kimbunga Dogo D alisema
"kimbunga mchawi jipange kuroga kwangu, wachawi wenzako wamekuwa wake zangu.....",  Kala pina kabuma hajui afanye nini, waambie waeusi navaa miwani na bado naona gere 
sikiliza wimbo wote hapa chini na alichokisema young killer na dogo d mwenyewe








Nilipata nafasi ya kuongea na Dogo D mwenyewe na hiki ndicho alichokisema
"Unajua mziki ni changamoto halafu mi pia nipo nao peace wote, Nay nipo nae peace, young killer na Mo Music wote nipo nao peace, halafu pia ngoma hiyo "wamenichokoza" imeongelea ukweli mtupu, maana Nay pia nikimpigiaga simu sometime hapokei, unajua Mo Music kipindi haijahit basi nenda tulikuwa nae peace ila ilivyohit basi nenda akabadilika so hii ngoma imeongelea ukweli asilimia kubwa sana na ndio maana ngoma hii inapenya na inazidi kupenya na nikaamua kuwachana ambao wanazingua siku zote"

nilipoongea na Young Killer alisema 

"kwa upande wangu kidogo nimechukulia kawaida kutokana na dogo amekaa aka create idea, ameangalia akaona idea flani ambayo inafaa kwa upande wake kwahiyo akaamua achane, ametuchana kwa respect hajavuka mipaka hajatudiss saaana kusema kwamba tuweze kujukua hatua labda tumpige kwasababu yule ni mdogo na sidhani kama anaweza kukaa akafikiria kunidiss indeep zaidi kutakana na mimi mwenyewe kuwa ni sehemu kubwa sana ya msaada wake kwahiyo naamini ni idea na wala hakuna tatizo lolote baina yangu mimi na yeye au hata hao wengi aliowachana.kwahiyo ni idea ya kawaida kabisa ametudiss kwa kutonyesha kabisa, hajavuka mipaka na nimechulia powa kwasababu mimi  hata ngoma iliyotoka kabla ya hii nimefanya nae, na hata kipindi anaifanya ngoma hii alinipigia akaniambia nimefanya ngoma hii na hii na akanitumia na nikaisikiliza so binafsi  nilimwambia fresh tu kutokana na idea, so binafsi haijanipain na nimeichukulia fresh tu naamini ni idea tu  kila kitu kinaenda kama kilivyopangwa yeaah"

nilipomtafuta Nay  alisema hataki kuongelea hiyo ishu