TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
BIA YA KIGO GOLD LAGER YA SERENGETI BREWERIES LTD YASHINDA TUZO YA MEDALI YA DHAHABU YA UBORA DUNIANI YA MONDE SELECTION.
Dar es Salaam, Septemba 8, 2014
BIA
ya Kibo Gold Lager imechaguliwa kuwa mshindi wa medali ya dhahabu kwa
ubora duniani inayotolewa na ‘Monde Selection’. Kibo ilipokea
utambulisho huo wa kimataifa wakati wa sherehe za 53 za kila mwaka
zilizofanyika huko Bordeaux, Ufaransa.
‘Monde
Selection’ ni tuzo zinazotolewa kila mwaka tangu mwaka 1961, kwa ajili
ya bidhaa za vinywaji na chakula. Huendeshwa na kampuni ya Biashara
ijulikanayo kama ‘International Institute for Quality Selections’ ya
Brussels, Ubelgiji. Bidhaa hizo huonjwa na kujaribiwa ili ziweze kupewa
alama ya ubora.
Akizungumza
baada ya kupokea tuzo hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia ya
Serengeti Breweries Ltd (SBL), Bw. Steve Ganon, alisema: “Kama familia
ya SBL, tumefarijika sana kusikia habari hii kubwa inayoihusu bidhaa
yetu, kitu kama hiki huwa
hakitokei hivi hivi; tumekifanya kitokee... Kwa hiyo ninaipongeza timu
nzima ya SBL kwa juhudi zao za kujenga imani kwa watumiaji.”
Bia
ya Kibo Gold ilizinduliwa miaka 15 iliyopita chini ya Kibo Breweries.
Kwa bahati mbaya, bidhaa hiyo haikudumu sana sokoni kutokana na kufungwa
kwa kampuni ya Kibo Breweries. Nembo hiyo ilichukuliwa na Serengeti
Breweries Ltd na kuzinduliwa upya Juni 2012 katika kiwanda cha SBL
kilichopo Moshi Brewery ambako ndiko huzalishwa na kusambazwa
sehemukubwa ya kaskazini mwa Tanzania katika mikoa ya Kilimanjaro,
Arusha, Tanga na Manyara, kati ya mingine mingi.
Lengo
la bia ya Kibo Gold ni kutanua wigo wa vinywaji vya Serengeti Breweries
Ltd na kuwashika watumiaji wa daraja la kati katika soko la kaskazini
mwa nchi.
Agosti
2013, Kibo Gold ilibadilishwa na kuwekwa katika chupa yenye shingo
ndefu maarufu kama ‘mwanamke nyonga’ ili kwenda na wakati na matakwa ya
soko la kisasa.
Sasa
Kibo ipo katika chupa yenye shingo ndefu ya milimita 500 ikiwa na
asilima 5.5 ya kileo inayodumu kwa kipindi cha miezi sita. Kauli mbiu ya
Kibo ni ‘Yaone maisha katika mwanga bora.’
Bia hii kwa sasa inauzwa rejareja kwa Sh 1,800