Ni muda sasa kumekuwa na taarifa za msanii Baby Madaha kuonekana sana jijini Dsm badala ya kuwa Kenya ambako ndo anafanya kazi zake za music chini ya lebo ya Candy n Candy huku kukiwapa mashaka mashabiki wake wengi.
Baby Madaha amezungumzia issue ya kuwepo zaidi Bongo na kuwatoa wasiwasi mashabiki wake.
Akizungumza na Zenj Fm Radio Baby madaha alisema yupo huku ingawa kazi zinaenda poa kutoka na utandawazi hivyo akitakiwa kuwa Kenya anaenda fasta na kurudi tena Bongo.