BONGOCLAN Tanzania

Website yetu ipo katikamatengenezo

Copyright © BongoClan Tanzania™ | Published By Gooyaabi Templates | Powered By Blogger
Design by WebSuccessAgency | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com

HABARI ZILIZOSOMWA SANA WIKI HII

Wema ni kweli anavuta Bangi???


Super Star kunako tasnia ya sinema za Kibongo, Jacqueline Wolper Massawe (26), anadaiwa kuangua kilio kisa kutopata mtoto.
 
Kwa mujibu wa chanzo makini ambacho ni mtu wake wa karibu, staa huyo amekuwa akihaha kusaka mtoto huku shinikizo likitoka kwa bibi yake, mzaa baba ambaye amekuwa akimuuliza juu ya yeye kumpata mtoto kwani umri unazidi kuyoyoma.
 
Habari zilidai kwamba mwanadashosti huyo alishakwenda kwa madaktari mbalimbali ambao walimtaka kutokuwa na pupa kuhusiana na suala hilo na zaidi azidi kumuomba Mungu.
 
“Unajua umri ukishasogea, wanawake wengi huwa na wasiwasi juu ya suala hilo la kupata mtoto kama ilivyo ishu ya kusaka ndoa maana ni kati ya vitu vinavyowatesa.
 
“Wolper ana wataalam wake lakini hawajamwambia kama ana tatizo la kutopata mtoto.
 
“Kuna maelekezo ambayo wamekuwa wakimpa ambayo humrejeshea furaha anapowaza ishu hiyo.”
 
“Madaktari walimwambia tatizo la kutopata ujauzito ina maana mwanaume na mwanamke au watu walio katika uhusiano wa kutafuta ujauzito ndani ya mwaka mmoja wameshajitahidi kufanya hivyo lakini wameshindwa.
 
“Walimwambia pia inaweza ikawa zaidi ya mwaka mmoja lakini wastani kiwango cha chini ni mwaka mmoja ambacho Wolper alishakuwa na mwanaume lakini hakufanikiwa ndiyo maana wakati mwingine anakuwa na hofu.
 
“Kuna wengine wanamwogopesha wanapomwambia kukosa mtoto ni tatizo kubwa katika jamii kwani kila mwanamke  anataka afikie malengo ya kuwa na familia na hasa kunapokuwa na shinikizo la wazazi wanataka mjukuu.
 
“Katika maelezo yao, madaktari walimwambia si mwanamke pekee anayeweza kuwa na tatizo bali hata mwanaume, hivyo tatizo linaweza kuwa kwa hao wanaume aliowahi kuchepuka nao,” chanzo kilimaliza kutiririka huku kikiomba hifadhi ya jina.
 
Baada ya kujazwa data hizo, Risasi Jumamosi lilimsaka Wolper ambapo alipopatikana, alifunguka kila kitu juu ya ishu hiyo.
 

Akizungumza  mara tu baada ya kutua Dar kwa ndege akitokea mkoani Kilimanjaro ambako alikwenda kumsalimia bibi yake huko Old Moshi, staa huyo alisema kwamba hakuna siku ambayo aliumia kama alivyokwenda kijijini na kukutana na bibi yake na kuanza kumuuliza kuhusu lini atapata mtoto.
 
“Kiukweli hakuna kitu ambacho kiliniingia kwenye moyo kama bibi yangu kuniuliza kuhusu mtoto, nimejikuta nikitoa machozi tu. Ni kama alitonesha kidonda,” alisema mdada huyo.
 
Wolper alisema kuwa bibi yake alimsisitiza kwamba asijali kuhusu mtoto atakula nini  bali akimpata ampeleke kwake kwani atakula chochote atakachokula bibi huyo.
 
Katika maelezo mengine, Wolper alisema amejitahidi sana kutafuta mtoto lakini imeshindikana lakini anamuamini Mungu kuwa atampata kulingana na matakwa yake.
 
“Nimejitahidi sana kusaka mtoto lakini imeshindikana hivyo kwa wale ambao wanabahatika kupata mimba nawashauri wasitoe maana mtoto ni faraja kubwa kwa wanawake,” alisema Wolper.
 
Wolper aliongeza kwamba aliyachukua maneno ya bibi yake kwa mikono miwili na atayafanyia kazi, inawezakana mpaka mwakani anaweza kulikamilisha hilo lakini kuna changamoto moja tu anayokumbana nayo nayi ni  nani wa kuzaa naye ambaye atakuwa baba bora wa mwanaye.
 
“Unajua unaweza kuzaa mtoto wala isiwe tabu kumlea kabisa kwani wapo watu wengi wanaweza kumwangalia, tatizo ni nani wa kuzaa naye tu jamani,” alisema Wolper huku akiamini kuwa siku ikifika Mungu atamjalia mtoto.
 
Wolper aliwahi kuripotiwa kutoka kimapenzi na wanaume kadhaa wakiwemo mastaa wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Khalid Juma ‘Jux’ na yule mwanaume aliyezua naye tafrani kabla ya kumwagana, Abdallah Mtoro ‘Dallas’ na huyu wa sasa ambaye bado hajamuanika jina, wote eti wameshindwa kuzaa naye.
Chanzo: Risasi Jumamosi/Gpl